• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Songea waridhia ombi la kurekebisha bei za maji za SOUWASA

Imewekwa kuanzia tarehe: August 22nd, 2022

WANANCHI katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wameridhia kuhusu ombi la kurekebisha bei za huduma za maji lililotolewa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Songea(SOUWASA).

Wananchi hao wameridhia taftishi kuhusu ombi hilo katika kikao maalum kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea kilichoshirikisha wawakilishi kutoka makundi yote wakiwemo wananchi, madiwani na wenyeviti wa mitaa.

Licha ya kuunga mkono mapendekezo ya kurekebisha bei za maji,wananchi hao  wameiomba SOUWASA kuhakikisha wanaboresha miundombinu ya maji ikiwa ni Pamoja na kuongeza saa za wateja kupata maji.

“Sisi wananchi tunaunga mkono marekebisho ya bei za huduma za maji,hata hivyo tunaomba ongezeko hilo liende sanjari na kuboresha huduma zenu SOUWASA,tunapendekeza matumizi ya LUKU kwenye maji ili kupunguza malalamiko kwa wasoma mitana kuongeza mtandao wa majitaka mjini Songea,alisema  Mathew Ngalimanayo,Diwani wa Kata ya mjini Manispaa ya Songea.

Akizungumza wakati anafungua na kufunga  kikao hicho,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,Kanali Laban Thomas amewapongeza wananchi wa Manispaa ya Songea  kwa kujitokeza kwa wingi katika kikao hicho na kuridhia mapendekezo ya kurekebisha bei za huduma za maji za SOUWASA.

RC Thomas amesisitiza kuwa maji ni huduma nyeti kwa usitawi wa wananchi na uchumi na kwamba upatikanaji wa maji safi na ya kutosha ni kielelezo cha ubora wa Maisha ya watu.

“Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais  wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan  imekuwa ikifanya jitihada kubwa katika kufanya mabadiliko na maboresho makubwa katika sekta ya maji’’,alisema RC Thomas.

Hata hivyo amesema serikali imeongeza wawekezaji katika sekta ya maji ili kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji na kuhakikisha lengo la kutoa huduma ya maji kwa asilimia 95 mijini linatekelezwa ifikapo mwaka 2025.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa SOUWASA Mhandisi Patrick Kibasa  amesema hadi sasa Mamlaka yake imefanikiwa kutoa majisafi  kwa asilimia 86 na kwamba SOUWASA  ina mtandao wa kusambaza majisafi wenye urefu wa kilometa 522.5 ambapo wateja 20,266 wameunganishwa katika mtandao wa majisafi.

Hata hivyo ameyataja malengo ya SOUWASA ni kuongeza upatikanaji wa maji kutoka asilimia 86 hadi kufikia asilimia 95 mwaka 2025 na kupunguza upotevu wa maji kutoka asilimia 22 hadi asilimia 20 ifikapo mwaka 2025.

Naye Mjumbe wa Bodi ya EWURA Richard Kayombo amewapongeza wadau wa Songea kutoka makundi yote kushiriki kikamilifu katika kikao hicho na kuunga mkono hoja ya kurekebisha bei za huduma za maji.

“Wananchi waliopata fursa ya kuzungumza kwenye kikao hiki shida yao sio gharama ya maji,wanachohitaji ni upatikanaji wa majisafi katika maeneo yao ili kuondoa kero ya maji’’,alisema Kayombo.

Amesema utaratibu wa kupanga bei za maji nchini,huanza kwa Mamlaka ya Maji kuwasilisha maombi yake UWURA ambapo Mamlaka inaweza kufikia uamuzi wa kuomba ongezeko la bei na tozo ili kuweza kumudu gharama zilizopanda na kuongeza mtandao wa maji kwenye maeneo ambayo hayajafikiwa.

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati (EWURA)  imepewa jukumu la kudhibiti sekta ndogo ya Nishati,petroli,gesi asili na maji ambapo katika sekta ya maji na usafi wa mazingira EWURA inawajibika kudhibiti kiufundi na kiuchumi,utoaji wa huduma ya usambazaji wa maji na usafi  wa mazingira.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Agosti 22,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.