• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Tunduru waishukuru serikali kwa kuwasogezea huduma ya maji

Imewekwa kuanzia tarehe: March 16th, 2022

WANANCHI wa kijiji cha Chiwana na Umoja wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma,wameishukuru Serikali kwa kutimiza ahadi ya kuwapatia huduma ya maji safi na salama na kumaliza tatizo la miaka mingi la wananchi hao kutumia muda mwingi na umbali mrefu kutafuta maji kwa matumizi ya kila siku.

Wametoa kauli hiyo jana mara baada ya wakala wa maji na usafi wa mazingira (Ruwasa) kukamilisha kutekeleza mradi mkubwa wa maji ambao umeanza kutoa huduma kwa wananchi hao.
Akizungumza kwa niaba ya wenzake Jemshid Hamis alisema,wanawake wa kijiji hicho walikuwa waathirika wakubwa wa tatizo la maji safi na salama kutokana na kutembea umbali mrefu kutafuta maji kwa matumizi ya familia huku wakishindwa kufanya kazi nyingine za maendeleo.

Alisema, mradi huo wa maji umeleta faraja na matumaini makubwa kwa wananchi wa kijiji hicho ambapo tangu ulipoanza kufanya kazi umesaidia sana kumaliza kero ya huduma ya maji na sasa wananchi wanapata fursa ya kufanya shughuli za uzalishaji mali.

Kwa upande wake Mganga wa Zahanati ya Chiwani Jenifer Valentino alisema, kabla ya kufikishwa kwa maji safi na salama changamoto kubwa kwa wakazi wa kijiji hicho ilikuwa magonjwa ya kuhara na matumbo mara kwa mara kutokana na kutumia maji ya visima vya asili ambayo sio safi na salama.

Alisema, kwa sasa idadi ya watu wanaofika katika zahanati hiyo kutokana na kusumbuliwa na maradi hayo imepungua sana kutokana na matumizi ya maji ya bomba baada ya kukamilika kwa mradi wa maji uliotekelezwa na Ruwasa.
Hata hivyo,amewashauri wananchi wa kijiji hicho kuendelea kutumia maji ya bomba ambayo ni safi na salama kwa ajili ya matumizi yao ya kila siku, badala ya kutumia maji ya visima vya asili.

Naye Fundi Sanifu wa Ruwasa wilaya ya Tunduru Kassim Dinny alisema,mradi wa maji Chiwana ni kati ya miradi iliyotekelezwa kupitia mpango wa lipa kutokana na matokeo(P4R) kwa kuwatumia wataalam wa ndani.

Alisema,mradi maji Chiwana unahudumia vijiji viwili vya Chiwana na Umoja ambapo jumla ya wakazi wanaonufaika ni 4,281 na umegharimu jumla ya Sh. 182,531,648.88.
Alisema, kati ya fedha hizo Serikali kuu imetoa Sh.175,996,148.88,nguvu za wananchi Sh.6,535,500.00 ambapo mradi huo umetumia fedha zote zilizotengwa na Serikali,na Sh.14,036,567.72 zimeokolewa na kutumika katika kazi za nyongeza.

Kassim alitaja kazi zilizoongeza ni pamoja na kuongeza mtandao wa bomba umbali wa mita 1,265 na kufanya jumla ya mtandao wa bomba wenye urefu wa mita 4,765 na kujenga vituo vingine vinne vya kuchotea maji.
MWISHO.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.