• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI wahamasishwa kuanza ufugaji nyuki

Imewekwa kuanzia tarehe: February 28th, 2022

WANANCHI wa kata ya Mahanje na Mateteleka Halmashauri ya Madaba mkoani Ruvuma,wamehimizwa kuanza ufugaji nyuki kibiashara kwa kuwa hakuna gharama katika uendeshaji wake na ina faida kubwa pamoja na soko la uhakika.

Wito huo umetolewa jana na Mkuu wa Mkoa huo Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, wakati akizungumza na baadhi ya wakulima wa kata ya Mateteleka akiwa katika kampeni ya upandaji miti katika Jimbo la Madaba wilayani Songea.

“biashara ya ufugaji nyuki ni nzuri sana ikilinganisha na biashara nyingine kwani ukishaweka mizinga yako unasubiri nyuki waingie huku wewe unaendelea na shughuli za shamba na haulazimika kuamka asubuhi kuwatafuta nyuki na wakishaingia wanaanza kutengeneza asali ambayo unavuna mara mbili hadi tatu kwa mwaka”alisema Ibuge.

Jenerali Ibuge alisema, uzoezfu unaonyesha kuna watu wametajirika kutokana na kuuza asali ambayo ina soko la uhakika ndani na nje ya nchi tofauti na mazao mengine.

Amewataka wananchi kuchangamkia fursa ya ufugaji nyuki, kwani katika Halmashauri hiyo na kuna miti mingi inayowezesha biashara ya kufuga nyuki na kuuza asali kufanyika kwa tija, badala ya kuendelea kujikita kwenye mazao ambayo yanachangamoto nyingi ikiwamo ukosefu wa soko na bei.

Alisema,Serikali ina wajali na kuwathamini sana wananchi ndiyo maana imeanzisha utaratibu wa kutoa mikopo isiyo na riba kwa makundi ya vijana,wanawake na wenye ulemavu na kuwataka kujitokeza kuchukua mikopo ili waweze kuanzisha miradi mbalimbali ya kiuchumi.

“Ndugu zangu tumieni maeneo haya ya hifadhi kufuga nyuki,nyinyi ndiyo wanufaika na siyo mimi,jiungeni kwenye vikundi au mtu mmoja mmoja na wataalam wa TFS watawapa elimu ya namna bora ya ufugaji huo”alisema Jenerali Ibuge.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho, amewataka wakazi wa jimbo la Madaba hasa vijana kuacha kukimbilia mjini kwa ajili ya kufanya shughuli ambazo hazina manufaa ikiwamo kuendesha boda boda na kupiga debe stendi.

Amewaasa vijana,wabaki vijijini ambako kuna fursa nyingi na zenye tija kubwa kwa maisha yao na familia zao badala ya kukimbilia mjini ambako hakuna fursa zinazoweza kuwainua kiuchumi.
Alisema,ufugaji wa nyuki ni fursa mojawapo katika jimbo la Madaba na mkoa huo kwa ujumla kwani kuna maeneo yanayowezesha biashara hiyo kufanyika, na kama itatumika vizuri wananchi wataondokana na umaskini na kuchangia pato la Taifa.

Kwa upande wake Meneja wa wakala wa huduma za misitu Tanzania(TFS) Kanda ya Kusini Manyisye Mpokigwa alisema, wao kama wasimamizi wa misitu hapa nchini wako tayari kushirikiana kwa kutoa mizinga na mikopo ya fedha kwa watu walio tayari kuanza biashara hiyo.

Kwa mujibu wa Mpokigwa, TFS inaruhusu jamii kufuga nyuki katika misitu na maeneo yanayowazunguka na kuwataka wananchi kuunda vikundi vya ufugaji nyuki ili waweze kunufaika na fursa hiyo.
Alisema, ufugaji nyuki ni biashara nzuri ambayo imewaondoa watu wengi katika umaskini na bei ya asali lita 1 ni Sh. 10,000 hadi 15,000 ambapo mzinga mmoja unatoa lita 20 na kwa mwaka unavuna mara mbili.

Alisema,TFS ina mfuko maalum wa misitu ambao unatoa fedha kuanzia Sh.milioni 5 hadi milioni 50 kwa watu waliojiunga katika vikundi kwa ajili ya kuanzisha miradi ya kiuchumi ikiwamo ufugaji nyuki.
MWISHO.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.