• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI zaidi ya milioni mbili Kanda ya Songea wapata elimu ya sheria

Imewekwa kuanzia tarehe: February 4th, 2025

wananchi zaidi ya 2,206,169 kutoka mikoa ya Ruvuma, Njombe, Mtwara, na Lindi wamepata elimu ya sheria kupitia mabanda yaliyokuwa katika Soko Kuu Songea na vipindi vya redio za kijamii.

Hayo yamesemwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Songea Mheshimiwa James Karayemaha wakati anazungumza katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya sheria nchini  iliyoanza  25 Januari  25,2025 na kufikia tamati Februari  Mosi 2025. 

Mheshimiwa Karayemaha amesema Wiki ya sheria imelenga kupunguza hofu dhidi ya mfumo wa mahakama, majaji, mahakimu, polisi, na taasisi za kupambana na rushwa.

Maadhimisho ya mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu:

“TANZANIA YA 2050: Nafasi ya Taasisi Zinazosimamia Haki Madai Katika Kufikia Malengo Makuu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo.”

Jaji Mfawidhi amesisitiza umuhimu wa misingi ya haki na amani katika maendeleo ya taifa. Pia, amezitaka taasisi za haki madai kushirikiana kwa karibu kuhakikisha mfumo wa sheria unachangia kufanikisha Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050.

Wadau waliotoa mchango mkubwa katika wiki ya sheria ni pamoja na Jeshi la Magereza, Polisi, Mawakili wa Serikali, TLS, TAKUKURU, Zimamoto, Uhamiaji, Vodacom, NMB, NBC, na taasisi nyingine nyingi. 

Wadau hawa walihamasisha matumizi ya TEHAMA katika mfumo wa sheria, ikiwemo usajili wa mashauri kwa njia ya mtandao (e-CMS), usikilizaji wa mashauri kwa video conferencing, na mfumo wa TanzLII kwa upatikanaji wa nyaraka za kisheria.

Mahakama ya Tanzania imeahidi kuimarisha matumizi ya TEHAMA ili kufanikisha utoaji wa haki kwa haraka na kwa uwazi. Aidha, imesisitiza matumizi ya usuluhishi (mediation) kama njia mbadala ya kutatua migogoro kwa haraka, kuokoa muda na gharama za mashauri.

Miongoni mwa changamoto zilizotajwa zinazoweza kuathiri utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya 2050 ni pamoja na Ucheleweshaji wa mashauri,Rushwa na vitendo vya ukiukwaji wa maadili,Ukosefu wa elimu ya sheria kwa wananchi,Kukosa weledi katika kushughulikia migogoro ya walipa kodi na Ukosefu wa majengo ya mahakama na watumishi wa kutosha.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Songea, Mheshimiwa James  Karayemaha, amehimiza jamii kushiriki katika uandaaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050, akisisitiza kuwa maendeleo na ustawi wa jamii hayawezi kupatikana bila haki na amani.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.