• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANAOTUMIKISHA watoto mashambani Ruvuma kuchukuliwa hatua

Imewekwa kuanzia tarehe: February 3rd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas  amekemea tabia ya baadhi ya matajiri kuwatumikisha Watoto kwenye mashamba yao  na kuathiri masomo yao.

Akizungumza na wanahabari kwenye ukumbi wa  Mipango mjini Songea,Kanali Thomas amesema limeibuka tatizo la matajiri kuwatumikisha wanafunzi kwenye mashamba yao ambapo amewatahadharisha wenye tabia hiyo kuacha mara moja.

Mkuu wa Mkoa amewaagiza wakuu wote wa wilaya kuwachukuliwa hatua watu wote wanaoendelea kuwatumikisha watoto.

“Utumikishwaji wa Watoto sio tu unafanyika mashambani, imebainika katika soko kuu la Songea Watoto wanatumikishwa kuuza vifungashio muda wa jioni,nimeagiza Watoto wote watakaoonekana  wanauza vifungashio wakamatwe na kuwachukulia hatua waliowajiri kufanya kazi hiyo’’,alisisitiza Mkuu wa Mkoa.

Ametoa rai kwa wanahabari kutumia vizuri kalamu zao kwa kuibua maovu yanayoendelea likiwemo la kuwatumikisha Watoto wadogo kinyume cha sheria.

Veronika Komba Mkazi wa Kijiji cha Mpitimbi wilayani Songea amekiri wamiliki wa mashamba katika Kijiji hicho kuwatumikisha wanafunzi kupanda mahindi na kuweka mbolea na kuwalipa ujira wa shilingi 5,000 na kwamba tabia ya kuwatumikisha Watoto mashambani imeshamiri pia katika Kijiji cha Mgazini na Muhukuru hivyo kuathiri masomo kwa wanafunzi.

Utumikishaji watoto wadogo bado unaendelea nchini, licha ya serikali kuweka sheria ya kumlinda mtoto mwenye umri usiozidi miaka 18.

Sheria ya haki za mtoto ya mwaka 2009, inabainisha wazi kuwa mtu hataruhusiwa kumuajiri au kumshughulisha mtoto katika aina yoyote ya kazi itakayomnyonya mtoto.

Tanzania ni miongoni mwa nchi 174 zilizoridhia Azimio la Umoja wa Mataifa namba 182 la kukomesha utumikishaji watoto chini ya umri wa miaka 18.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amewataka wazazi na walezi ambao hawajawapeleka Watoto wao shule kuhakikisha wanawapeleka shule vinginevyo watachukuliwa hatua za kisheria.

Amesema hadi kufikia Januari 26,2024 asilimia 77.6 ya Watoto wa madarasa ya Awali walikuwa wameandikishwa,shule za msingi asilimia 91.1 na walioripoti kidato cha kwanza ni asilimia 60.9.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.