• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WATAALAM wa mifugo Nyanda za Juu Kusini walivyodhamiria kudhibiti magonjwa ya mifugo

Imewekwa kuanzia tarehe: September 28th, 2020

Wataalam wa mifugo Nyanda za Juu Kusini wameweka mikakati endelevu itakayosaidia kudhibiti magonjwa ya mifugo na kukuza uchumi na pato la Taifa.

 Mikakati hiyo imewekwa na wataalam hao katika Kikao cha wataalamu wa uvuvi na Mifugo kanda ya Nyanda za  Juu kusini kilichojumuisha mikoa mitano ya  Iringa,Mbeya,Njombe,Ruvuma na Songwe  na kufanyika kwenye ukumbi wa Songea klabu mjini Songea.

Akizungumza wakati anafungua kikao hicho mgeni rasmi Katibu Tawala Msaidizi Huduma za Uchumi na Uzalishaji n Jeremia ameyataja malengo ya kikao hicho kuwa ni  kujadili mikakati na changamoto  katika sekta ya ufugaji na Uvuvi.

Amesema changamoto zikipatiwa ufumbuzi wa kudumu zinaiwezesha sekta ya mifugo na uvuvi kusonga mbele  na iweze kufanya vizuri kwa kuinua pato la mtu mmoja mmoja na kuinua Uchumi wa Nchi.Sendoro amewapongeza Maafisa Mifugo na Uvuvi kwa kazi kubwa wanazofanya ,licha ya Halmashauri zote kuwa na uhaba wa maafisa ha ukilinganisha na mahitaji ya yaliyopo ambapo ametoa rai waendelea kupambana na kuhakikisha sekta ya mifugo inasonga inapata mafanikio makubwa.

Hata hivyo Katibu Tawala Msaidizi huyo amesema katika Sekta  hiyo kuna tatizo la magonjwa ya mifugo  na kwamba  mwananchi wa kawaida anategemea wataalamu  wa mifugo kuwapa  elimu sahihi na kuhakikisha Mifugo inakuwa na afya  nzuri.

“Kuna magonjwa yanayomaliza baadhi ya mifugo mfano kideri NA mdondo yanasababisha kuku kufa, kwa mwaka huu katika Mkoa wa Ruvuma kuku zaidi ya laki moja  wamekufa”,alisema Sendoro.Amewaomba wataalamu wa Mifugo kuhakikisha mifugo inaposafirishwa kutoka mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine wahakikishe wanachukua sampuli ili kujiridhisha vinginevyo ugonjwa utasambaa sehemu moja kwenda nyingine.

Sendoro amewashauri wataalamu wa mifugo kuchukua tahadhali ili kuhakikisha afya ya mifugo inakuwa salama na mfugaji hapati hasara na kupata mbegu bora za mifugo.Kwa upande wake Daktari wa mifugo wa  Mkoa wa Mbeya Samora Stanley  akizungumza katika kikao hicho ametoa rai kwa wafugaji kuangalia namna ya kutatua changamoto mbalimbali inayoikabili sekta hiyo.

 Meneja wa wakala wa Maabara Nyanda za Juu Kusini Dr.Kwali Bula amesema wameanagalia namna bora ya kudhibiti Magonjwa ya mifugo pamoja na  kutoa chanjo na uogeshaji wa mifugo.Amesema kila Halmashauri wamejiwekea utaratibu wa kuchanja mifugo na ukusanyaji wa Maduhuri wa Serikali za Mitaa  pamoja na Serikali kuu  kutoka kwa wataalamu wa kanda kutoka iringa, ambayo inategemewa zaidi kwa wanyama kama Nguruwe na Ngómbe wa Maziwa.

Imeandaliwa Aneth Ndonde

Kutoka ofisi ya Habari Mkoa wa Ruvuma

Septemba 28,2020

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.