• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WATEJA watano wa NMB washinda fedha taslimu milioni tano Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: April 5th, 2024

Wateja watano wa Benki ya NMB wamejinyakulia  fedha taslimu Sh.milioni moja kila mmoja katika Droo ya kila Mwezi iliyochezwa katika tawi la NMB Songea  kupitia kampeni kubwa inayofahamika kwa jina la Pesa Akaunti.

Wateja walioshinda Droo hiyo ya mwezi ni Alhami Shemkay ,Msimu Mwnyimvua, Abdala Msimu, Emanue Masawe ,na unior Mtweve.
Pesa akaunti ni Droo maalum inayoendeshwa na Benki hiyo ikihamasisha Watanzania kutumia Benki ya NMB kuweka fedha,kufungua akaunti,na kupata mikopo kwa ajili ya shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo kilimo.
Meneja wa mauzo wa NMB Kanda ya kusini Roman Degeleki amesema,akaunti ya Pesa Akaunti inafunguliwa kwa gharama ndogo kuanzia Sh.1,000 na haina kianzio cha fedha na mteja hapewi kadi badala yake anaunganishwa moja kwa moja na simu yake ya mkononi.
Amesema,akaunti hiyo inamwezesha mteja kufanya matumizi na malipo mbalimbali ikiwemo kulipa Luku,kununua King’amuzi,kulipa bili za maji na vitu vingine kulingana na mahitaji ya mteja husika
Kulingana na Meneja huyo,kupitia Pesa akaunti mteja  anaweza kuchukua mkopo hadi Shilingi laki tano kupitia simu yake ya mkononi bila kuweka dhamana yoyote na kurejesha mkopo huo kwa kutumia simu yake.
Degeleki ametaja,faida nyingine ya Pesa akaunti kuwa ni  mteja kupata Bima ya simu ambayo ikipata changamoto yoyote Benki ina uwezo wa kuifanyia matengenezo simu hiyo bila kujali gharama zake.
Ametoa rai kwa Watanzania,kuchangamkia fursa hiyo kwa kuendelea kufungua akaunti na kuweka fedha kwenye Benki ya NMB ili waweze kunufaika na huduma zinazotolewa katika kila Wilaya na Mkoa hapa nchini.
Kaimu meneja wa NMB Tawi la Songea Mwalimu Mbwambo amesema,Droo ya mwezi imewahusisha  wateja ambao waliweka fedha kwenye akaunti zao kuanzia kiwango cha fedha kisichopungua Sh.50,000.
Kwa upande wake Mkaguzi na Mdhibiti wa Michezo ya kubahatisha kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Salim Bugufi amesema,kampeni hiyo inafanyika chini ya uangalizi wa Bodi hiyo ili kujiridhisha mtu anayepata fedha hizo kuwa ni mteja halali ya NMB.
Mkazi wa kijiji cha Ligera wilayani Namtumbo Silaji Mango,ameipongeza Benki hiyo kwa kuendesha Droo hiyo ambayo imehamasisha watu wengi kutumia Benki ya NMB kwa kufungua akaunti na kuweka fedha.Mango,amewasihi washindi wa Droo hiyo kutumia fedha walizopata kuwekeza katika shughuli muhimu za maendeleo kama vile kilimo na mifugo badala ya kuzitumia kwenye mambo ya anasa.




Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.