• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WATENDAJI wa Halmashauri Songea watakiwa kutenga fedha za kutekeleza afua za lishe

Imewekwa kuanzia tarehe: July 6th, 2021

Mkuu wa Wilaya Songea Mkoani Ruvuma Pololeti Mgema ametoa agizo kwa viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma kutenga fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya kutekeleza afua za lishe katika Halmashauri hiyo.

Mgema ametoa agizo katika kikao cha tathimini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe kilicho fanyika hivi karibuni   katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma.

Mgema ametoa agizo hilo kufuatia viashiria vya lishe kutotekelezeka kwa ufanisi katika jamii ambapo Serikali ngazi ya Mkoa hadi Watendaji wa Vijiji walisaini mkataba mwaka 2019 wa utekeleza wa afua za lishe kwa lengo la kufanikisha mapambano dhidi ya lishe duni tatizo  ambalo bado lipo katika jamii.

“Ukweli ni kwamba lishe ni swala mtambuka na utapiamlo ni matokeo ya mkusanyiko wa matatizo mengi, “amesisitiza Mgema.

Mgema amefafanua kuwa Serikali inatambua umuhimu wa kuwekeza kwenye lishe kama msingi imara na mkakati wa kufanikisha shughuli za kiuchumi ambazo zitatuwezesha kufikia uchumi wa kati wa viwanda endapo tu wananchi wake watakuwa na afya bora na wenye uwezo wa kufanya kazi.

Mgema ameyataja matokeo ya lishe duni ni utapiamlo ambao unasababishwa na ulaji duni,maradhi mbalimbali,kukosa uhakika wa kupata chakula katika jamii,matunzo duni kwa mama mjamzito tangu siku ya kutunga mimba hadi kujifungua ,mazingira duni ,machafuko ya kisiasa,mgawanyo wa rasilimali  usio zingatia uwiano wa kijinsia na mazingira machafu.

Mgema amezitaja baadhi ya afua za lishe ambazo zinatakiwa kutekelezwa na hazitekelezwi ipasavyo katika kupambana na tatizo la lishe duni kwenye jamii kuwa ni utapia mlo mkali,upimaji wa watoto sehemu ya juu ya mkono,utekelezaji wa vikao vya kisheria vya lishe,usimamizi shirikishi wa lishe,na utoaji wa matone ya vitamini A kwa watoto chini ya miaka mitano

Mgema ameyataja makundi ambayo yanaonekana kuathirika na tatizo la lishe duni kuwa ni Watoto chini ya miaka mitano ,wanawake walio katika umri wa kuzaa wa miaka 15-49,wanawake wajawazito ambao baadhi yao  wanakabiliwa na changamoto ya kujifungua watoto njiti na wenye mtindio wa ubongo na upungufu wa damu.

Ameongeza kwa kusema takwimu zinaonyesha kuwa Halmashauri inatatizo la udumavu wa asilimia 37.4, uzito pungufu upo kwa asilimia 13, ukondondefu asilimia 18.5, uzito mkubwa kwa wanawake na wanaume ni asilimia 21.1 na upungufu wa damu kwa akinamama wenye umri wa kuzaa ni asilimia 14, na Watoto chini ya miaka mitano ni asilimia 21.

Kwa upande wake Afisa lishe wa Halmashauri hiyo Joyce Kamanga amesema lishe sasa ni swala kimaendeleo Nchini mapambano dhidi ya lishe duni ni moja ya maeneo ya kipaumbele ya miaka mitano (2016/17-2020/21); mpango wa unaolenga kutekeleza Dira yetu ya maendeleo ya mwaka 2025.

Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma inawatoto elfu 21 ambao wanatakiwa kutengewa fedha kwaajili ya utekelezaji wa afua za lishe kwenye ngazi ya Kata ambako ni kitovu cha utekelezaji wa afua hizo.

Imeandaliwa na kuandikwa na

Jacquelen Clavery

Afisa Habari Songea dc.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.