• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WATUMISHI hospitali ya Rufaa ya Mkoa Songea walivyoshiriki katika maombi ya kutokomeza corona

Imewekwa kuanzia tarehe: April 18th, 2020

WAFANYAKAZI wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma wametekeleza maagizo ya Rais Dkt.John Magufuli kwa kufanya maombi ya kutokomeza virusi vya corona hapa nchini.

Rais Magufuli ametoa rai kwa watanzania wote kufanya maombi maalum ya kuliombea Taifa kwa siku tatu dhidi ya virusi vya corona ambavyo vinasumbua dunia nzima.

Akizungumza kabla ya maombi hayo, Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma Dr.Yona Mwakabumbe amewaasa madaktari na wauguzi kufanya kazi kwa tahadhari ili kuepuka maambukizo ya corona.

Dr.Mwakabumbe amesema hospitali hiyo ipo katika hatua za mwisho za kupata mashine maalum ya kupima joto la mwili (Thermal scanner) na kwamba kuanzia Aprili 20 mwaka huu kazi ya kupima joto kwa kila mtumishi atakayekuwa anaingia katika hospitali hiyo itaanza rasmi.

Kwa upande wake Muuguzi Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Hilda Ndambalilo amepongeza kitendo kilichofanywa na wafanyakazi wa hospitali hiyo kufanya maombi maalum ya kukabiliana na corona.

Ndambalilo amesema katika janga la kukabiliana na corona, madaktari na wauguzi ni askari waliopo mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya corona na kwamba kwa kufanya maombi na kujikabidhi kwa Mwenyezi Mungu anaamini  watashinda vita hiyo.

“Tutashinda kwa kishindo kikubwa katika vita hii tukijikabidhi katika maombi kwa Mwenyezi Mungu,sisi ndiyo jeshi linalotegemewa katika mapambano haya,muhimu ni kujikinga na kuchukua tahadhari,’’,alisisitiza Ndambalilo.

Dr.Mathayo Chanangula ni Daktari Msaidizi  na Padre wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Ruvuma akizungumza katika maombi hayo amesema kila kitu kimeumbwa na Mungu na kwamba hata wadudu wa COVID 19 wameumbwa na Mungu na kwamba Mungu ana mamlaka ya kuwazuia na kuwatokomeza.

“ Tufanye maombi ya siku tatu kama alivyotuelekeza Rais wetu , tumuombe Mwenyezi Mungu aseme COVID 19 sasa basi,tutashinda’’,alisistiza.

Rais Dkt.John Magufuli ametoa rai kwa watanzania kufanya maombi  maalum ya siku tatu kuanzia Aprili 17 hadi 19 kufanya maombi maalum ya kuliombea Taifa dhidi ya virusi vya corona ambavyo ni janga la Dunia.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Aprili 17,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.