• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAWEKEZAJI wakaribishwa kuwekeza katika kilimo Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: February 19th, 2025

SERIKALI Wilayani Songea Mkoa wa Ruvuma imesema,itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji wa ndani na nje ya Nchi watakaohitaji kuwekeza na kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo Wilayani humo.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Songea Kapenjama Ndile, baada ya kutembelea shamba la kahawa lenye ukubwa wa zaidi ya hekta 3,000 linalomilikiwa na Kampuni ya Aviv Tanzania Ltd ambalo linazalisha asilimia zaidi ya tano ya kahawa inayolimwa hapa nchini.

“Kampuni ya Aviv Ltd tangu ilipoanza shughuli zake imekuwa na mchango mkubwa kiuchumi,kwa mfano mwaka jana imelipa mapato ya Sh.milioni 700 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Songea kutokana na mauzo ya kahawa,fedha hizi zimekwenda kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo kwa Wananchi”alisema Ndile.

Alisema kuwa,hayo ni maendeleo makubwa hivyo Serikali ya Wilaya kwa kushirikiana na Halmashauri zake itajenga na kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji hao ili wasikutane na vikwazo kwa kushindwa kulipa mapato na kusababisha Halmashauri kushindwa kujiendesha.

Ndile, amesifu kahawa inayozalishwa katika shamba la Aviv Ltd lililopo kijiji cha Lipokela Halmashauri ya Wilaya Songea kuwa ni tamu ikilinganishwa na kahawa inayolimwa kwenye mikoa mingine hapa nchini kutokana na radha yake.

Alisema,Wilaya ya Songea ni kimbilio kubwa kwa wawekezaji kutoka ndani na nje ya Tanzania wanaokwenda kuwekeza kwenye sekta ya kilimo kutokana na kuwa na mazingira rafiki ikiwemo ardhi nzuri inayofaa kwa ajili ya kilimo cha mazao mbalimbali ya chakula na biashara.

Kwa mujibu wa Ndile,Wilaya ya Songea ni Wilaya Mama kwa uzalishaji wa chakula katika Mkoa wa Ruvuma na ndiyo ghala kuu la Hifadhi ya Chakula Tanzania,hivyo amewaomba wawekezaji kwenda kuwekeza kwanikuna maeneo na mazingira mazuri yanayofaa kwa ajili ya shughuli za uwekezaji.

Dc Ndile amemtaja mwekezaji mwingine ni kampuni ya Ndolela Farm inayofanywa shughuli zake katika Halmashauri ya Madaba ambayo imepewa hekta 500 kwa ajili ya kilimo cha zao la mahindi na ngano inayotumika kama chakula na kutengeneza bia za kampuni ya Serengeti.

“siku za nyuma kulikuwa na kasumba kwa wawekezaji kuchukua malighafi za kutengeneza bia kutoka nchini Afrika Kusini wakati hapa nchini kuna malighafi za kutosha,hali hii imewarudisha nyuma wakulima wetu na wengine kukata tamaa ya kuendelea na uzalishaji wa zao hilo”alisema.

Alisema,kampuni ya Serengeti imeingia makubaliano ya kuwapa wakulima mbegu za shahiri ambao watazalisha na kuuza kwa kampuni hiyo ambapo Halmashauri ya Madaba itapata mapato na wakulima kupata watapata fedha kutokana na kilimo cha zao hilo.

Kwa upande wake Meneja uzalishaji wa Shamba la Kahawa la Aviv Hamza Kassim alisema,wakati wa msimu wa mavuno wana ajiri watu 4,000 hadi 5,000 kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini.

Hamza alisema,uwepo wa shamba hilo unasaidia Wananchi kupata ajira za muda na ajira za kudumu na kuchangia mapato ya Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Songea,Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA).

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.