• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZAZI Tunduru waishukuru serikali kwa fedha za ujenzi wa madarasa

Imewekwa kuanzia tarehe: June 6th, 2023

BAADHI ya wazazi wa kata ya Mchangani Halmashauri ya wilaya Tunduru,wameishukuru Serikali kutoa Sh.milioni 66.3  ili kujenga vyumba viwili vya madarasa katika shule ya msingi Changani ambayo inakabiliwa na upungufu mkubwa wa madarasa.

Wamesema,fedha hizo zinakwenda kupunguza msongamano wa watoto wao hasa wanaosoma elimu ya awali kukaa zaidi ya 60 katika chumba kimoja cha darasa.

Said Msusa alisema,madarasa hayo yatakapokamilika yatawasaidia watoto kukaa kwa nafasi na kuongeza usikivu darasani na hivyo kufanya vizuri katika masomo yao.

Aidha alisema,ujenzi wa madarasa mapya yatahamasisha hata wanafunzi watoro kupenda kusoma kwa kuwa kutakuwa na mahali pazuri kwa ajili ya kujifunzia tofauti na sasa ambapo watoto wanalazimika kukaa dawati moja zaidi ya watatu.

Amina Mkandu,amempongeza Raid Dkt Samia Suluhu Hassan kutokana na jitihada zake za kutafuta fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ambazo zinatumika kuboresha huduma mbalimbali za kijamii.

Alisema madarasa hayo mapya  ya elimu ya awali,yatahamasisha watoto kwenda shule kupata elimu na kuwataka wazazi na walezi kuhakikisha wanatumia fursa  ya ujenzi wa vyumba bora vya madarasa kupeleka watoto wao shule.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Neema Lubida alisema,wamepokea kiasi cha Sh.milioni 66.3 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mawili ya elimu ya awali kupitia mradi maalum wa uboreshaji wa mazingira ya ufundishwaji kwa elimu ya awali na msingi (Boost).

Alisema,katika shule hiyo ni jumla ya watoto ni 674 wanaohitaji  vyumba 15 vya madarasa,lakini yaliyopo ni 10 hivyo mradi huo utakapokamilika utasaidia kupunguza tatizo hilo.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Mchangani Hairu Mussa alisema,katika muda wa miaka miwili ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan wilaya hiyo imepokea zaidi ya Sh.bilioni 231.9 ambazo zimekwenda kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Alisema,kama Halmashauri ya wilaya wanaendelea kupambana katika suala la ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kumaliza  baadhi ya changamoto zinazowakabili wananchi katika maeneo mbalimbali wilayani humo

Alieleza kuwa,katika shule hiyo kuna watoto zaidi ya 84 wa elimu ya awali ambao kwa sasa wanatumia chumba kimoja cha darasa,hivyo kupatikana kwa mradi huo ni faraja kubwa siyo kwa Halmashauri tu bali hata kwa wazazi na jamii nzima ya wana Tunduru.

Hairu ambaye ni mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru,amewaomba wazazi kupeleka watoto shuleni ili kupata haki yao ya msingi, badala ya kuwaacha nyumbani  au kuwakimbizia mashambani.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.