• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZAZI washauriwa kuwaunganisha watoto wao na CHF

Imewekwa kuanzia tarehe: June 9th, 2022

WAZAZI na walezi mkoani Ruvuma,wametakiwa kuwapa misingi Bora watoto wao waliopo shuleni kwa kuwaunganisha na mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) ili waweze kuwa na uhakika wa kupata matibabu pindi wanapougua.

Wito huo umetolewa na Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF)mkoani Ruvuma Hance John, wakati akizungumza katika kikao maalum cha wazazi wenye watoto wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Wasichana Mbinga(Mbinga Girls) wilayani Mbinga.

Hance alisema, zawadi bora kwa watoto ni pamoja na kuwaunganisha katika mfuko huo kwani utamwezesha kuwa na uhakika wa matibabu akiwa shuleni, badala ya usumbufu wa kurudi nyumbani ili wazazi wampeleka Hospitali, au kuwabebesha mzigo walimu kutumia fedha zao kwa ajili ya kuwalipia wanafunzi gharama za matibabu wanapokwenda katika vituo vya kutolea huduma za afya.

“Serikali yetu inawataka Watanzania wote wakiwamo wanafunzi kujiunga na mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ili wawe na uhakika wa kutibiwa kwa wakati,ubora na kwa bei nafuu,nawaomba sana wazazi wenzangu hakikisheni mnawakatia Bima za afya watoto wenu”

Alisema,mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ni shirika la umma lenye wajibu wa kuwahudumia Watanzania wote bila kubagua wakiwamo watoto walio chini ya umri wa miaka 18 ambapo mzazi atatakiwa kujaza fomu zinazopatikana kwenye shule husika.

Kwa mujibu wa Hance,suala la matibabu kupitia mfuko wa Taifa wa Bima aya Afya ni jambo muhimu kwani hata tunapozungumzia suala la maendeleo haliwezi kupatikana kama watu hawatakuwa na afya njema.

Alisema,Wilaya ya Mbinga na mkoa wa Ruvuma kwa jumla umebarikiwa kuwa na ardhi nzuri inayofaa kwa kilimo cha mazao mbalimbali na watu wanaofanya kazi kwa kujituma,hivyo sio rahisi wazazi kukosa fedha kwa ajili kuwaunganishwa watoto na NHIF.

Alisema, kwa kawaida mwanafunzi mwenye afya iliyotetereka hawezi kuwa msikivu darasani jambo linaloweza kumuathiri na kufanya vibaya katika masomo na mitihani yake kwa sababu atatumia muda wa masomo kwenda Hospitali au kukaa nyumbani.

Alisema,suala la Bima ya afya hasa kwa wanafunzi wanaokaa Bweni ni muhimu kwani litapunguza usumbufu kwa walimu kutumia fedha zao kuwalipia wanafunzi gharama za matibabu badala ya gharama hizo kubebwa na wazazi.

Aidha,ameupongeza uongozi wa shule ya Sekondari Kigonsera kwa kuweka utaratibu ambao unamtaka kila mwanafunzi anayejiunga na shule hiyo awe na kadi ya matibabu ya mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, mkakati uliosaidia sana wanafunzi wake kufanya vizuri kitaaluma.




Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.