• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZEE Ruvuma waiomba serikali kutoa pensheni kwa wazee wote

Imewekwa kuanzia tarehe: January 30th, 2024

WAZEE wa Mkoa wa Ruvuma wameiomba serikali kuona uwezekano wa kutoa pensheni kwa wazee wote ili waweze kukabiliana na ugumu wa Maisha.

Wazee hao wametoa ombi hilo kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas kwenye kikao cha   wawakilishi wa wazee kutoka wilaya zote chenye lengo la  kusikiliza kero mbalimbali  zinazowakabili  wazee kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Akizungumza kwenye kikao hicho Mzee Christoms Makukula ameshauri serikali kutoa pensheni kwa  wazee wote kwa kuwa hivi sasa baadhi ya wazee  bado wanatekeleza majukumu ya kulea wajukuu ambao wameachiwa na vijana wao.

Makukula amezitaja changamoto za wazee kuwa ni kukosa matibabu kutokana na gharama kubwa  na kukosa fedha  za matumizi hivyo kuishi katika mazingira magumu.

Mzee Flavina Henjewele amekemea mmomonyoko wa maadili kwa vijana ambapo amesema hivi sasa baadhi ya vijana wanatumia dawa za kulevya  na kuvaa mavazi  ambayo ni kinyume na mila na desturi za Mtanzania.

Mzee Yohana Mbalale amesema kutokana na changamoto nyingi zinazowakabili wazee ameshauri  watumishi waliostaafu zamani waongezewe pensheni kwa kuwa fedha wanazopata ambazo ni chini ya shilingi laki moja hazitoshi kulingana na ugumu wa Maisha kwa kuwa wazee hivi sasa wanasomesha wajukuu na kuwalea.

Mbalale ameshauri kundi la wazee liwe na wawakilishi Bungeni kama ilivyo kwa watu wenye ulemavu,wanawake na vijana ili waweze kutetewa kwenye vyombo vyenye maamuzi.

Bibi Veronika Komba ameiomba serikali kutoa ulinzi wa kutosha kwa wazee ambao baadhi ya vijana wanawatuhumu kuwa ni wachawi, pia amewashauri wazazi na walezi kuwahimiza Watoto wao Kwenda makanisani na misikitini ambako watajengwa kiroho na kuepuka vitendo viovu.

Chifu wa Tano wa Kabila la Wangoni Imanuel Zulu amelitaja tatizo kubwa la vijana ni kuacha mila na desturi za Kitanzania na kuiga utamaduni wa kigeni  ambapo amewataka wazazi na walezi kukemea vitendo hivyo.

Akizungumza baada ya kusikiliz kero na maoni ya wazee Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas  ameahidi kufanyia kazi kero na mapendezo hayo huku akiwataka wazee hao kuwa mstari wa mbele kukabiliana na mmomonyoka wa maadili kwa vijana kwa kuwa vijana wamewazaa na wanaishi nao ambapo amesisitiza jamii nzima inahusika kukabiliana changamoto za vijana.

“Wazazi na walezi msilalamike kuhusu mmomonyoko wa maadili kwa watoto,badala yake chukueni hatua kwa sababu Watoto hao ni wenu,sote tunatakiwa kukemea maadili mabovu kwa Watoto wetu ambao ni wazazi wa kesho’’,alisisitiza.

Amesisitiza kuwa vijana wengi wamepoteza malezi na hawaendi misikini na makanisani hali inayosababisha kuacha kutenda matendo mema yanayompendeza Mwenyezi Mungu hivyo kutokuwa na hofu na Mungu

Kuhusu pensheni kwa wazee,Mkuu wa Mkoa amesema wazo hilo amelichukua na ataliwasilisha kwenye Mamlaka zinazohusika waangalia uwekezakano wa kutoa pensheni kwa wazee wote.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma anaendelea na ziara ya kusikiliza kero na maoni ya makundi mbalimbali mkoani Ruvuma hatimaye kutafutia ufumbuzi

Pichani kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas akiwa na  Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma wakisikiliza kero na maoni ya wazee wa Mkoa wa Ruvuma 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.