• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZIRI ashauri Halmashauri ya Songea kutenga maeneo ya ufugaji wa samaki

Imewekwa kuanzia tarehe: July 17th, 2023

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb)  ameshauri watendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Songea kuanza kutenga maeneo yatakayosaidia wananchi kujishughulisha na utengenezaji wa Mabwawa ya ufugaji wa samaki ambayo yatachochea uchumi na kuongeza wigo wa mapato kwa Halmashauri.

Kauli hiyo ameitoa wakati alipotembelea kujionea Mradi wa Shamba Darasa la Ukuzaji wa Viumbe Maji unaoendelea kujengwa na serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Kata Mpitimbi Halmashauri ya wilaya ya Songea.

Waziri Mhagama ameridhishwa na hatua ya ujenzi wa shamba la darasa la ukuzaji wa viumbe hai, amesema tunaweza kutumia mabwawa ya ufugaji wa samaki kama chanzo cha ajira na uchumi kwa wananchi wa Mpitimbi B.

“Mhe. Rais, Dkt, Samia Suluhu Hassan anamaono ya mbali sana, ametupatia mradi ambao utasaidia kuzalisha mbegu na mafunzo, tunatakiwa tuanze kujiandaa kwa kutengeneza mabwawa”.

Amefafanua mradi utakapokamilika; wananchi wawe na miundo mbinu yao ya mabwawa ya ufugaji wa samaki tayari, ili mafunzo yatakapokuwa yanafanyika wawe wanachukua vifaranga na kuweka kwenye mabwawa yao, alisema Waziri Mhagama.

Tunaweza tukatumia mikopo ya Halmashauri kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kuweza kutengeneza mabwawa yao ya ufugaji wa samaki, alisisitiza.

“tunapaswa tuwe na mabwawa Mengi ya samaki kushoto na kulia mwa eneo la mradi yatakayomilikiwa na vijana wakinamama na wazee ambayo samaki watafugwa kisasa na watakuwa na uzito mzuri alisema,” Waziri Mhagama.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Songea Mhe. Menas Komba amesema Halmashauri inaanda andiko la kimkakati kwa ajili ya kupata fedha ya kuendeleza Lambo kubwa la maji lilopo katika kijiji cha Mpitimbi B ambalo linahitaji fedha Zaidi ya million 500.

Amefafanua kwamba ujenzi wa lambo hilo utaenda sambamba na Halmashauri kutaratibu kupitia Halmashauri ya kijiji maeneo ambayo wananchi watajenga mabwawa ya kufugia samaki, alisema

Awali katika taarifa Mhandisi Msimamizi wa Mradi, kutoka Halmashauri ya Songea Bi,Flora Tairo alisema Mradi uko katika hatua ya ukamilishwaji, kwa majengo na upandaji nyasi kwenye kingo za mabwawa. ambapo amesema  mradi  huo  utakapokamilika utakuwa na mabwawa manne, uzio, darasa la mafunzo, stoo pamoja na maliwato.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.