• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZIRI MKUU aridhishwa na miundombinu hospitali ya Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: January 6th, 2023

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema ameridhishwa na maboresho yaliyofanyika katika hospitali ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa Oktoba 18, 2022 alipofanya ziara hospitalini hapo.


Mheshimiwa Waziri Mkuu alipofanya ziara katika hospitali hiyo na alieleza kutorishwa na milango iliyowekwa na kuagiza iondolewe na iwekwe mingine yenye viwango na leo Januari 06, 2023 amekagua maendeleo ya utekelezaji wa agizo na ameridhishwa na kazi iliyofanyika.


Kufuatia utekelezaji huo Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na utekelezaji wa maelekezo hayo ambapo hadi sasa jumla ya milango 67 kati ya 84 imeondolewa na kuwekwa mipya yenye ubora.


“Leo nimeona milango bora kabisa, kwa nini tulikubali kuweka milango mibovu wakati mizuri ipo? Hii haikubaliki kwa sababu tunapoteza fedha za Serikali zinazotokana na kodi ya wananchi. Ni lazima kila mtumishi wa umma atimize wajibu wake.”


Amesema Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ya afya ili kusogeza huduma muhimu za kijamii karibu na wananchi.


Pia, Waziri Mkuu amewataka Wakuu wa Idara katika halmashauri zote nchini wasimamie kikamilifu utekelezaji wa shughuli zote za maendeleo katika maeneo yao ili kuhakikisha fedha zinazoidhinishwa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa miradi zinatumika ipasavyo.


“Haipendezi kuona viongozi wakuu waje na kubaini madudu katika miradi wakati watendaji mpo. Kila mtumishi awajibike ipasavyo katika eneo lake ili kuhakikisha lengo la Mheshimiwa Rais Dkt. Samia la kuwaletea maendeleo wananchi linatimia.”


Mradi wa ujenzi wa hospitali hiyo unatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 7.5, mpaka sasa hospitali hiyo imepokea shilingi bilioni 4.2 kutoka Serikali kuu ambapo majengo 20 yameshajengwa, majengo 13 yamekamilika, majengo saba yapo katika hatua za ukamilishaji. Hospitali itakapokamilika inatarajia kuhudumia watu Zaidi ya 200,000.


Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Festo Dugange amesema Serikali ya awamu ya sita itaendelea kuiboresha sekta ya afya ikiwemo kununua magari mawili kwenye halmashauri zote 184 nchini ikiwa moja nila wagonjwa na linguine ni kwa ajili ya usimamizi wa huduma za afya.


Akizungumza kuhusu ujenzi wa shule ya sekondari ya wasichana ya Namtumbo, Dkt. Dugange amesema watahakikisha wanasimamia maagizo yote yaliyotolewa na Waziri Mkuu ili kuhakikisha shule hiyo inakamilika kwa wakati na inaanza kudahili wanafunzi


Awali, Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Dkt. Christopher Wabarumi aliishukuru Serikali kwa kuendelea kuboresha huduma za afya katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo na wilaya hiyo ambayo inaendelea na ujenzi wa majengo ya 22 katika hospitali ya wilaya hiyo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.