• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZIRI MKUU aziagiza Mamlaka za serikali za Mitaa kutenga bajeti kuhifadhi maeneo ya kihistoria

Imewekwa kuanzia tarehe: February 27th, 2021

WAZIRI Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa ameiagiza mikoa na Mamlaka zote za serikali za mitaa kutenga bajeti ya kuyahifadhi maeneo yote ya kihistoria ili kutopoteza historia yake kwa manufaa ya Taifa.

Majaliwa ametoa agizo hilo katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Innocent Bashungwa kwenye kilele cha tamasha la kumbukizi ya miaka 114 ya vita ya Majimaji lililofanyika kwenye viwanja vya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji mjini Songea.

Waziri Mkuu pia ameiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kuendelea kuadhimisha kumbukizi hizo ili ziwe sehemu ya vivutio vya utalii nchini ambazo zinachangia kuongeza pato la Taifa na kwamba Wizara hiyo kwa kushirikiana na Wizara ya Habari zihamasishe na kuelimisha jamii fursa za kumiliki maeneo ya malikale.

Akizungumzia mashujaa wa vita ya Majimaji ,Waziri Mkuu ameagiza kumbukumbu zilizopo ndani ya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji zinaendelea kuhifadhiwa ili kujenga uzalendo na kuleta utaifa kwa kizazi  kilichopo na kijacho.

“Mkoa wa Ruvuma hivi sasa una makumbusho mawili ambayo ni Makumbusho ya Majimaji na Makumbusho ya Dkt.Hayati Rashid Mfaume Kawawa,Mkoa huu ndiyo kitovu cha kusaidia wanaharakati wa ukombozi wa Afrika hususan nchi jirani ya Msumbiji’’,alisisitiza Waziri Mkuu.

Kwa upande wake Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Songea mjini Dkt.Damas Ndumbaro  akizungumzia kumbukizi ya miaka 114 tangu kunyongwa mashujaa wa vita Majimaji,amesema maadhimisho hayo yamelenga kuenzi ushujaa  wa wazee wetu katika harakati za awali za ukombozi dhidi ya wakoloni.

“Maisha ya wazee wetu ni fahari yetu kwa sababu wazee hawa walipigania nchi kwa uzalendo wa hali ya juu,ukombozi wa mwafrika una historia kubwa sana hapa kwa sababu mapambano yaliyofanyika kwa muda mrefu zaidi dhidi ya mkoloni nchini Tanzania yalifanyika Songea’’,alisema Dkt.Ndumbaro.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Christawaja Ntandu  ameyataja malengo ya tamasha la kumbukizi ya mashujaa wa majimaji ambalo hufanyika kila mwaka kuwa ni  kukumbuka na kuwaenzi mababu zetu ambao walinyongwa Februari 27,1906 na kuzikwa kwenye makaburi mawili ndani ya makumbusho ya Majimaji.

Hata hivyo amesema tamasha hilo hutoa fursa kwa wananchi kutunza,kuenzi na kuendeleza uzalendo,amani na mshikamo ambao umerithiwa kutoka kwa mababu zetu na kwamba tamasha hilo pi hutumika kuibua na kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo ukanda wa kusini.

Naye Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa Dkt.Noel Lwoga amesema wazee waliopigana katika vita ya Majimaji miaka 114 iliyopita dhidi ya wakoloni walitoa mchango mkubwa katika kutetea taifa letu na kwamba vita ya Majimaji imebeba utajiri mkubwa wa historia ya ukombozi na uhuru wa nchi yetu.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Februari 27,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.