• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZIRI wa Katiba akabidhi vifaa tiba Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: December 29th, 2024

Waziri wa Katiba na Sheria na Mbunge wa Jimbo la  Songea mjini, Dkt. Damas Ndumbaro, amekabidhi vifaa tiba vya utengamao katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Songea (HOMSO) vyenye thamani ya shilingi milioni 10.

Katika hafla ya kukabidhi vifaa hivyo ambayo imefanyika katika Hospitali hiyo, Dkt. Ndumbaro amesema maombi ya kupata vifaa hivyo ambayo yalitolewa na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Songea Dr. Magafu Majura yanakidhi vigezo vya kuchochea maendeleo ya wananchi.

"Endapo mwananchi atatibiwa haraka na kupata nafuu na kupona kabisa atarudi kwenda kufanya kazi zake za kimaendeleo na hiyo ndio tafrisi ya kuchochea maendeleo,"alisema Dkt. Ndumbaro.

Ameongeza kuwa wanufaika wa vifaa hivyo sio watu wa Jimbo la Songea mjini pekee bali ni wa majimbo yote ya mkoa wa Ruvuma hadi nchi jirani ambao wanafika kutibiwa katika hospitali hiyo kwa kuwa idara ya utengamao imekuwa ikuhudumia wagonjwa wengi.

Naye Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Dr. Chihoma Mhako, ameeleza kuwa uwepo wa kitengo hicho katika hospitali ya mkoa umesaidia wagonjwa wengi ambao walikuwa wakipelekwa rufaa kwenye hospitali za kanda Mbeya au Mtwara.

Naye Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Songea, Dr. Magafu Majura ameeleza kuwa Idara ya Utengamao katika hospitali hiyo inatoa huduma ya utengenezaji na ukarabati wa viungo saidizi, matibabu ya kurekebisha na kuzuia ulemavu, huduma baada ya upasuaji wa mifupa, misuli na mishipa ya fahamu pamoja na kutoa Elimu ya kuzuia ulemavu na utengamao kwa wateja na jamii.

Amebainisha kuwa kwa mwaka 2023/24  Idara ya Utengamao imehudumia wagonjwa 7,171 ambapo ni wastani wa wagonjwa 590 kwa mwezi ambao wamekuwa na matatizo ya mgongo kwa muda mrefu, kiharusi , utindio wa ubongo, mguu kifundo, mishipa ya fahamu na maumivu mbalimbali ya viungo na misuli.

Vifaa tiba hivyo vilivyokabidhiwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Songea (HOMSO) vimenunuliwa na fedha iliyotoka katika mfuko wa kuchochea maendeleo jimboni.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.