• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZIRI wa Maji awaomba wakuu wa mikoa kusimamia miradi ya maji

Imewekwa kuanzia tarehe: July 6th, 2021



Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amewaomba Wakuu wa mikoa na Makatibu Tawala wa mikoa kushirikiana katika usimamizi wa miradi ya maji nchini.


Mhe. Aweso amesema hayo katika kikao cha mafunzo ya uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa ya Tanzania Bara kinachofanyika jijini Dodoma.


Amesema Wizara ya Maji imedhamiria kuhakikisha lengo la kumtua mama ndoo ya maji linafikiwa kama lilivyoelekezwa na serikali.

"Niwaombe viongozi tushirikiane kwa dhati kuhakikisha tunaondoa changamoto zote za upatikanaji wa huduma ya majisafi. Peke yetu hatutaweza." Aweso amesema.


Pamoja na hilo amepokea mapendekezo mbalimbali kutoka kwa viongozi hao wa mikoa na kuwaahidi kuyafanyia kazi.


“Kuhusu kuwa na utaratibu wa wadau wa maji kukutana na kujadili masuala mbalimbali yanayohusiana na sekta ya maji ni jema sana.

Naomba nipokee ushauri wenu wa jinsi ya kulitekeleza ili liwe endelevu. Isiwe ni maelekezo ambayo yanaweza kubadilishwa na kiongozi mwingine. Liwe ni muongozo rasmi na utamaduni ili hata kiongozi ajaye, afanye hivyohivyo" Aweso amesema.


Amesisitiza kuwa Wizara ya Maji haitakuwa kikwazo katika kufikia malengo. Amezitaja baadhi ya hatua zilizochukuliwa na Wizara ili kuimarisha usimamizi wa miradi ya maji kuwa ni pamoja na uamuzi wa kuingia makubaliano na Chuo cha Maji ili kuwatumia wahitimu wa chuo hicho katika usimamizi na uendeshaji wa miradi ya maji nchini.


Wakuu hao wa mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa ya Tanzania Bara wanashiriki mafunzo ya uongozi Jijini Dodoma.

Imeandikwa na Afisa Habari Wizara ya Maji Dodoma





Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.