• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WILAYA tano za Mkoa wa Ruvuma kunufaika na umeme wa REA

Imewekwa kuanzia tarehe: August 12th, 2021

WILAYA tano mkoani Ruvuma zinatarajia kunufaika na mradi wa umeme wa REA awamu ya tatu utakaogharimu zaidi ya shilingi Bilioni 70 ifikapo Desemba mwaka huu.

Hayo yalisemwa hivi karibuni na waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani wakati alipokuwa akizungumza na wananchi kwenye uzinduzi wa mradi huo uliofanyika kimkoa katika kata ya Nalasi wilayani Tunduru mkoani Ruvuma.

Dkt. Kalemani alizitaja wilaya zitakazonufaika na mradi huo wa umeme wa REA awamu ya tatu kuwa ni Tunduru,Namtumbo,Songea,Mbinga pamoja na wilaya ya Nyasa.

Akizungumza katika uzinduzi wa mradi huo waziri huyo alisema kuwa serikali ya awamu ya sita imedhamiria kufikikisha umeme huo wa REA kwenye vijiji na vitongoji vyote vilivyosalia katika wilaya hizo ndani ya miezi 18.

Aidha amewataka wananchi hao kutumia fursa hiyo ya kuingiza umeme huo kwa gharama ya shilingi 27,000 katika kuanzisha viwanda vidogo vidogo kwa lengo la kuchochea uchumi wa mtu mmoja mmoja pamoja na kuiingizia serikali mapato.

Hata hivyo waziri Kalemani ametoa maagizo na maelekezo mbalimbali kwa kandarasi zinazotekeleza mradi huo ikiwa pamoja na kuacha kuruka kijiji,kuacha kuwatoza wananchi gharama za nguzo,kuacha kubagua nyumba za kuingiza umeme na kuhakikisha Tanesco inafungua ofisi kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi kwenye maeneo hayo.

Naye mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Balozi wilbart Ibuge amemshukuru na kumpongeza waziri Kalemani kwa jitihada zake za kuhakikisha wananchi wa vijiji mbalimbali mkoani humo wanafikiwa na huduma hiyo huku akitoa rai kwa jamii kuacha tabia ya kuharibu miundombinu ya umeme kwa madai kwamba yeyote atakayebainika kufanya hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi(CCM)mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho alisema kuwa chama chake kinafurahishwa kuona serikali ikiendelea kutekeleza Ilani ya chama hicho ambayo waliahidi kwa wananchi wakati wa uchaguzi mkuu uliopita.

Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Tunduru kusini Daimu Mpakate amemshukuru rais Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo ambapo katika kata ya Nalasi jimboni humo umeme huo unatarajiwa kuwashwa Agosti mwaka huu.

Imeandikwa na Julius Konala

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.