• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WILAYA ya Nyasa yapitisha bajeti ya shilingi bilioni 27

Imewekwa kuanzia tarehe: February 17th, 2023

Baraza  la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa,  tarehe 14/02/2023 limepitisha Bajeti ya  yenye thamani ya shilingi bilioni 27,653,395,441.07,  kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya Halmashauri, katika  kikao kilichofanyika , Ukumbi Kepten John Komba Uliopo Mbamba bay Wilayani Nyasa.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Bw. Stewart Nombo,  ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza la Madiwani amesema kuwa baraza  limeidhinisha mpango na bajeti ya maendeleo, kwa mwaka wa fedha 2023/2024, kwa kuwa bajeti hii imelenga kutatua kero mbalimbali za wananchi, ikiwa ni pamoja na kutekeleza Miradi ya Maendeleo, na kutoa wito kwa  madiwani  kutoa ushirikiano kwa wataalamu katika usimamizi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Kata zao.

Akiwasilisha Mapendekezo ya Mpango wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2023/ 2024,  Kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji Wilaya ya Nyasa, Mkuu wa Divisheni ya Mipango na uratibu Bw. Chrstopher Ngonyani amesema, kuwa bajeti hiyo, inalenga 

Program mbalimbali zilizopangwa kufanyika katika Halmashauri. Kati ya Kiasi hiki Tsh 16,000,575,951.07 ni matumizi ya kawaida,Tsh 15,196,594951.07 ni mishahara na Tsh 803,981,000.00 ni matumizi mengineyo (OC)Tss 10,068,182,000.00 ni matumizi ya miradi ya maendeleo (Tsh 4,110,371,000.00 ni fedha za ndani na Tsh 5,957,811,000.00 ni fedha za nje na Tsh 1,447,627,190,000.00 ni fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri, kati ya fedha hizo tsh 994,923,000 ni mapato halisi(proper Own Source Tsh 452,704,190.00 ni mapato lindwa na michango ya nguvu ya jamii ni tsh 137,000,000.00.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Bw Jimson Mhagama,  amewataka madiwani wa Wilaya ya Nyasa kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao, kwa kushirikiana na wananchi, kutekeleza miradi hiyo na kusema kuwa Miradi hii inatekelezwa kwa fedha za walipa kodi, kwa hiyo ni jukumu la kila kiongozi kusimamia fedha hizo ili kujiletea maendeleo.

“waheshimiwa  madiwani ninawataarifu kuwa kila ninapokuandikia na kukupa taarifa za kukuletea fedha katika eneo lako, ni jukumu lako kusimamia, kuwashirikisha wananchi, na kutekeleza miradi kwa ubora wa hali ya juu, kwa kuwa fedha zinazotekeleza miradi hii ni kodi za wananchi wetu na Mh Rais amezileta ili zitatue changamoto za wananchi hivyo kila kiongozi anatakiwa kuwajibika kwa nafasi yake” .

Naye Mbunge wa Jimbo la Nyasa Mhandisi Stella Manyanya,  amesema Wilaya ya Nyasa inakusudia kujenga uwanja wa kisasa mkubwa wa michezo ili kuongeza utalii na kuhamasisha michezo .

Aidha  amepongeza Mkurugenzi wa Mtendaji wa Wilaya ya Nyasa Bw Jimson Mhagama, na Wataalamu wake, walioshiriki kuandaa mpango na bajeti  ambayo imezingatia vigezo  muhimu vyenye lengo la kutatua Kero za wananchi Wilayani Hapa

Naye Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mh.Filbetho sanga alijitambulisha katika baraza hilo na kuwaeleza kuwa ameanza kazi katika Wilaya ya Nyasa na ameagiza Uwepo wa ulinzi na Usalama na kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza wanaripoti haraka kwa asilimia 100.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.