• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WILOLESI FOUNDATION yakabidhi vifaatiba hospitali ya Rufaa ya Mkoa ,Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: December 6th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Bi. Mary Makondo amekabidhiwa vifaa tiba vyenye thamani ya milioni 10,450,000 na Taasisi ya WILOLESI Foundation vitakavyowasaidia watoto wachanga wanaozaliwa na changamoto mbalimbali katika Hospitali ya Mkoa, Songea (HOMSO).

Makondo amekabidhiwa vifaa hivyo katika hafla iliyofanyika Hospitali ya Mkoa,Songea (HOMSO) iliyopo mjini Songea, ambapo ameishukuru Taasisi hiyo kwa kufanikisha upatikanaji wa vifaa hivyo.

"Tunawashukuru na kuwapongeza sana taasisi ya  WILOLESI Foundation kwa kuwa na maono na kufanikisha shughuli ya mbio za hisani zilizolenga kupata fedha za kusaidia ununuzi wa vifaa tiba kwa ajili ya kusaidia watoto waliozaliwa na changamoto mbalimbali," alisema Makondo.

Amebainisha kuwa Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya Afya ikiwemo miundombinu, rasilimali watu, dawa na vifaa tiba lakini bado wanatambua mchango wa wadau wengine kama WILOLESI Foundation katika kuunga mkono jitihada za Serikali hasa katika kuboresha afya za watoto wachanga.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Dr. Louis Chomboko, amesema wanapokea vifaa hivyo vilivyotolewa na WILOLESI Foundation na vitatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Ameongeza kuwa wanaendelea kufanya juhudi mbalimbali ndani ya mkoa ili kukabiliana na changamoto zinazowapata watoto wachanga wanapozaliwa, ambapo asilimia 62 ya hospitali 18 za Mkoa mzima zinatoa huduma ya kusaidia watoto wachanga wanapopata changamoto na takribani asilimia 48 ya vituo vya afya vinavyotoa huduma ya upasuaji navyo vinasaidia watoto hao.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa, Songea, Dr. Revocatus Makaranga, akitoa taarifa ya kitengo cha watoto wachanga kwa mgeni rasmi amesema kitengo hicho kinalaza na kuhudumia watoto takribani 80 kwa mwezi, ambao ni watoto waliozaliwa kabla ya wakati, waliopata homa ya manjano baada ya kuzaliwa na waliozaliwa baada ya miezi tisa na kupata changamoto mbalimbali za afya.

Vifaa hivyo vilivyokabidhiwa na WILOLESI Foundation ni Radiant warmer iliyogharimu shilingi milioni 5,900,000, CPAP Machine milioni 3,800,000 pamoja na Wheelchair with table laki 750,000 na kufanya jumla kuwa milioni 10,450,000.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.