• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WWF yatoa elimu na vifaa kukabiliana na tembo waharibifu Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: October 7th, 2021

SHIRIKA la kimataifa WWF limetoa elimu na vifaa kwa kukabiliana na tembo waharibifu katika vijiji vitano vilivyopo Halmashauri ya Namtumbo mkoani Ruvuma.

Akizungumza wakati anamkabidhi vifaa hivyo,Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Mhifadhi na Melimishaji wa WWF Ally Thabiti Mbugi  amesema wametoa elimu ya kujikinga na wanyama waharibifu hususan tembo kwa wananchi ili kukabiliana na uharibifu bila kuleta madhara kwa wanyama.

Mbugi amesema licha ya elimu,WWF pia imetoa msaada wa  vifaa mbalimbali vitakavyotumika kama nyenzo ya kukabiliana na tembo waharibifu ambapo vifaa aina ya vilipuzi 400 vimetolewa kwa wilaya ya Namtumbo.

Amevitaja vifaa vingine kuwa ni magunia ya pilipili,vilipuzi kamba na vitambaa vya pamba ambavyo vinatumika katika utengenezaji wa wigo wa pilipili ambao unasaidia kuzuia tembo wasiharibu mashamba ya wananchi.

‘’Hivi sasa tunakaribia msimu wa kilimo hivyo tumetoa elimu na vifaa mapema kabla ya uharibifu kufanyika,hata hivyo katika Mkoa wa Ruvuma tutatoa vilipuzi 800 katika wilaya za Namtumbo na Tunduru ambapo kuna uharibifu wa mazao unaofanywa na tembo,pia tumetoa mbegu za pilipili ili wananchi mwakani wasipate tabu’’,alisema.

Akizungumza  mara baada ya kupokea  vifaa hivyo Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Dkt.Julius Ningu amewapongeza na kuwashukuru WWF kwa msaada huo kutokana na ukweli kuwa Namtumbo imeathirika na wanyamapori waharibifu wa mazao.

‘’Ukiangalia mkulima mtaji wake ni nguvu zake mwenyewe,na anafanya kilimo cha msimu, hivyo wanyama wanapoharibu mazao ni pigo kwake’’,alisisitiza.

Amesema msaada uliotolewa na WWF serikali na wananchi wanauthamini na wataifanyia kazi iliyokusudiwa na kwamba serikali itashirikiana na wananchi kuhakikisha wanyama waharibifu wanarejeshwa kwenye maeneo yao ya asili.

Amesema ameshukuru elimu na msaada huo kutekelezwa kabla ya msimu wa kilimo hivyo inatoa nafasi kwa serikali kuwaandaa wananchi  pamoja na namna ya kuvitumia vifaa vilivyoletwa ili vitumike kwa tija.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Oktoba 6,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.