• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WWF yazindua elimu ya uhifadhi kwa shule za msingi Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: May 17th, 2022

JAMII nchini, imetakiwa kujenga mazoea ya kuwahusisha watoto wenye umri mdogo katika shughuli za maendeleo ikiwamo utunzaji wa mazingira na ulinzi wa rasilimali zilizopo kwa manufaa ya nchi yetu.

Wito huo umetolewa  kwa nyakati tofauti na Afisa Mhifadhi wa shirika la Kimataifa la utunzaji mazingira(WWF-Tanzania) Deogratius Kilasara, wakati akizungumza na wanafunzi wa shule ya Sekondari Namwinyu na Matemanga wilayani Tunduru  akiwa katika  uhamasishaji wa mpango wa elimu ya uhifadhi  mazingira mashuleni.

Alisema,sehemu mojawapo ya kufikisha ujumbe haraka kwa jamii nzima ni kuhusisha watoto hasa wenye umri mdogo kwani wao ndiyo wanaoshika sana wanachoambiwa au kusikia tofauti na watu wazima.

“Hawa watoto ukiwaambia kitu wanabeba hivyo kilivyo kupeleka kwa jamii,sio kama watu wazima ambao wana mambo mengi kichwani,ndiyo maana WWF kama wadau wa uhifadhi mazingira baada ya kutambua hilo tumeona ni vyema katika mpango wetu wa mwaka huu tuanze  na watoto waliopo shule za msingi na sekondari”alisema Kilasara.

Alisema, katika mpango huo wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari wataunda klabu  za mazingira zitakazofahamika kwa jina la Miyombo Klabu ambapo  watafundishwa namna ya kutunza mazingira,mapori na maeneo yaliyohifadhiwa ambako wanyama  pori wanapatikana.

Alisema,lengo ni kutoa elimu kwa wanafunzi ili waweze kufahamu umuhimu kuhifadhi na kutunza wanyamapori ambao kama wakitunzwa  vizuri  Taifa litapata faida nyingi zinazotokana na utalii wa uwindaji na  utalii wa picha.

Aidha alisema, elimu hiyo itawawezesha wanafunzi kushiriki moja kwa moja kusaidia katika suala zima la kutunza mazingira wakiwa katika umri mdogo na kufanikisha malengo na mipango iliyokusudiwa.

Alisema,shule zitakazohusika kwenye mpango huo zitaanzishwa bustani za miche ya miti kwa kuamini kwamba miche hiyo itasaidia kuibadilisha jamii dhidi ya vitendo vya  uharibifu wa mazingira.

Kilasara alieleza kuwa,wameanza kutoa elimu na mafunzo kwa wanafunzi  wa shule za msingi na Sekondari katika wilaya ya Namtumbo na Tunduru  na wataendelea  katika wilaya ya Liwale  na Rufiji ambako WWF wanafanya shughuli zao  na hadi sasa wamefanikiwa kuzifikia shule 30.

 Mhifadhi wa Mamlaka ya usimamizi wa wanyamapori Tanzania(Tawa) Ashura Hassan alisema,wameshatoa elimu ya kukabiliana na wanyama wakali na waharibifu katika vijiji mbalimbali vinavyozunguka mapori na maeneo yaliyohifadhiwa ambapo sehemu kubwa washiriki walikuwa watu wazima.

Alisema,kwa sasa wameona  ni vyema wakafika mashuleni ili wanafunzi nao waweze kufahamu umuhimu wa kutunza mazingira na kulinda  rasilimali za nchi yetu kama vile wanyama na misitu katika maeneo yao ambapo TAWA inatoa elimu  ya kujilinda na wanyama wakali na waharibifu hususani Tembo wanaovamia mashamba na kuharibu mazao.

Aidha,amewataka wananchi kuacha kulima ua kufanya shughuli zozote za kibinadamu kwenye maeneo ya hifadhi ili kuepuka  madhara makubwa yanayoweza kutokea.

Kwa upande wake Afisa Uhusiano wa Hifadhi ya Taifa ya Nyerere anayesimamia mahusiano ya ujirani mwema katika wilaya ya Tunduru Stephen Mpondo alisema, wanatoa elimu kwa jamii ili waweze kuheshimu na kutunza hifadhi zilizopo kwa faida ya jamii nzima.

Alisema,kuna sababu kubwa ya wanyama waharibifu hususani Tembo kuvamia makazi ya wananchi wanaoishi kuzunguka hifadhi hiyo na kufanya uharibifu,kula mazao na hata kujeruhi wananchi pindi wanapojaribu kuwafukuza ili warudi katika hifadhi.

Alisema, sababu mojawapo ni jamii kwenda kufanya shughuli zao ndani ya hifadhi ikiwamo kilimo na ufugaji,hivyo elimu hiyo  ina lenga kuwasaidia namna bora ya kuepukana na wanyama wakali na waharibifu,pamoja na kujilinda kwa kutumia njia mbadala ikiwamo kulima mazao yasiyopendwa kuliwa na wanyama.

Mwanafunzi wa shule ya Sekondari Namwinyu Tabia Mtua alisema,elimu hiyo itawasaidia kujilinda na wanyama wakali kama Tembo ambao wanapatikana kwa wingi katika maeneo  yao kutokana na kupakana na Hifadhi ya Nyerere.

Imeandikwa na Albano Midelo

wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Mei 17,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.