• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

YALIYOJIRI wakati RC Ibuge anampa pole Askofu Jimbo la Tunduru Masasi

Imewekwa kuanzia tarehe: August 8th, 2021

MKUU wa mkoa wa Ruvuma Brigadia Jenerali Wilbert Ibuge, amewataka viongozi wa Dini mkoani humo, kuchukua tahadhari wakati wa ibada kwa kuvaa Barakoa na kunawa mikono  wakati wote wa ibada ili kujinga na ugonjwa wa Corana.

Jenerali Ibuge ametoa kauli hiyo  alipokutana na Askofu wa Kanisa Katolki Jimbo la Tunduru- Masasi Mhashamu  Filbert Mhasi, kwa ajili ya kumpa pole kufuatia  kifo cha  Naibu Askofu wa Jimbo hilo Marehemu Castor Msemwa aliyefariki mwaka 2018.

Aidha amewaomba viongozi  hao kusaidiana na Serikali kutoa elimu  juu ya ugonjwa huo kwa wananchi  na  waumini wao, badala ya kazi hiyo kuiachia Serikali hasa ikizingatia kuwa viongozi wa Dini wana nafasi kubwa ya kukutana na kufikisha elimu kwa jamii kwa haraka.

Amesema, anatambua juhudi mbalimbali zinazofanywa na viongozi wa Dini katika wilaya hiyo na mkoa wa Ruvuma kwenye mambo mbalimbali ya imani na maendeleo,hata hivyo bado wana wajibu wa kuendelea kuelimisha jamii  kuchukua tahadhari ya ugonjwa huo.
Aidha Jenerali Ibuge,amewaomba  viongozi wa madhehebu ya Dini kuendelea kushikamana na kutoa elimu kwa wananchi wetu kuhusu tishio la ugaidi lililoanza kujitokeza katika mpaka wetu na Nchi jirani ya Msumbiji.

Amesema,suala la ulinzi wa mipaka yetu ni la kila mtu, kwa hiyo kama tukilegea kidogo inaweza kuathiri hata kwetu  hivyo amesisitiza ni lazima tuzuie  tishio la aina yoyote na kuhakikisha usalama wa nchi yetu unadumishwa ili kutoa nafasi kwa wananchi  kuendelea  kufanya shughuli zao za maendeleo.Amewataka viongozi wa Dini, kuwaelimisha wananchi  kutoa taarifa kwa vyombo vya ulinzi na usalama pale  wanapoona kuna dalili za mtu au kikundi cha watu wasioeleweka  katika maeneo yao kwani Serikali haiwezi kuweka wanajeshi kila mahala, lakini wananchi kama watatoa taarifa mapema itasaidia sana kuchukua hatua dhidi ya matukio ya aina hiyo.

Pia Jenerali Ibuge, amelishukuru Kanisa Katoriki Jimbo la Tunduru-Masasi kwa namna ambavyo limeendelea kutoa huduma mbalimbali kwa jamii kitu ambacho kina tija na ustawi mkubwa kwa wananchi na Nchi kwa jumla.

Amesema, mara nyingi binadamu wana tabia ya kusifia vitu baada ya kupita na ndiyo wanavikumbuka,lakini ni  vyema kutiana moyo na kutambua jitihada ambazo zinazofanyika na Kanisa Katoriki za kuunga mkono  juhudi za Serikali za kuwaletea wananchi maendeleo.Kwa upande wake Askofu wa Kanisa hilo Filbert Mhasi, ameishukuru Serikali ya wilaya na  mkoa kwa kuwa bega kwa bega na kanisa hilo wakati wote wa msiba wa Askofu Msemwa na wakati wa kusimikwa kwake kuwa Askafu wa  Jimbo hilo mwaka 2019.
Amesema, yeye kama kiongozi wa  Kanisa Katoliki Jimbo la Tunduru-Masasi ataendelea kushirikiana na serikali katika shughuli zote za maendeleo kwa ajili ya ustawi wa waumini,wananchi na Taifa.
Amesema,anatambua kazi kubwa inayofanywa na viongozi wa Serikali  za kuleta maendeleo kwani kwa muda mfupi amewaona jinsi wanavyoangaika kuhusiana na suala la elimu katika jamii ya wana Tunduru ambayo bado iko nyuma sana  hususani kwa watu wa kike.

Amesema, kwa nyakati tofauti viongozi  wa Serikali wakiongozwa na Mkuu wa wilaya hiyo Julius Mtatiro wanapita vijijini na wakati mwingine kulazimika kwenda hadi mstuni kuwasaka watoto waliacha shule ili waweze kuendelea na masomo. TAZAMA HABARI KWA KINA HAPAhttps://www.youtube.com/watch?v=ieiIHbnOAzI














ReplyForward






Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.