• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MIRADI ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 156 katika shule za sekondari

Start Date: 2022-10-31
End Date: 2023-03-31

5.2.5 Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo katika utekelezaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa ya kidato cha kwanza 2023.

Mkoa wa Ruvuma ulipokea fedha nje ya bajeti TShs.3,120,000,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 156 vya kidato cha kwanza 2023 katika shule za sekondari. Mchanganuo wa Fedha hizo ni kama inavyoonesha kwenye jedwali namba 7.

Jedwali Na. 7: Mchanganuo wa Fedha za Mpango wa Maendeleo kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya kidato cha kwanza 2023.

 

HALMASHAURI
IDADI YA VYUMBA VYA MADARASA
MGAO WA FEDHA
VILIVYOKAMILIKA
HATUA YA UKAMILISHAJI
ASILIMIA
TUNDURU DC

10

200,000,000.00

10

0

100

MBINGA DC

10

200,000,000.00

0

10

0

MBINGA TC

11

220,000,000.00

6

5

52

NAMTUMBO DC

17

340,000,000.00

3

14

17.6

SONGEA DC

10

200,000,000.00

7

3

95

MADABA DC

10

200,000,000.00

1

9

10

NYASA DC

12

240,000,000.00

8

4

67

SONGEA MC

76

1,520,000,000.00

0

76

0

JUMLA

156

3,120,000,000.00 

35

121

22.4

 

Hadi kufikia tarehe 30 Novemba, 2022 jumla ya vyumba 35 vya madarasa vimekamilika sawa na asilimia 22.4 na vyumba 121 vipo hatua za ukamilishaji.

 

5.2.6 Mapokezi ya fedha za ujenzi wa vituo vya afya na nyumba za watumishi kwa halmashauri

Mkoa umepokea jumla ya TShs. 980,000,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya vitatu na nyumba nne za watumishi wa halmashauri. Fedha hizi zimetokana na ruzuku ya serikali kuu na mapato ya ndani ya Halmashauri ikiwa ni jitihada za kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma bora karibu na maeneo yao. Mchanganuo wa fedha ni kama inavyonesha kwenye jedwali namba 8.


Jedwali Na 8. Mapokezi ya Fedha za Ujenzi wa Vituo vya Afya na nyumba za watumishi wa halmashauri

HALMASHAURI
IDADI VITUO VYA AFYA
KIASI CHA FEDHA KWA VITUO VYA AFYA
IDADI YA NYUMBA ZA WATUMISHI
KIASI CHA FEDHA NYUMBA ZA WATUMISHI 
SONGEA MC

0

0

0

0

TUNDURU DC

0

0

0

0

MBINGA DC

1

250,000,000.00

4

390,000,000.00

SONGEA DC

0

0

4

240,000,000.00

NYASA DC

1

50,000,000.00

0

0

MADABA DC

1

50,000,000.00

0

0

MBINGA TC

0

0

0

0

NAMTUMBO DC

0

0

0

0

JUMLA 

3

350,000,000.00

8

630,000,000.00

Miradi mingine inayotekelezwa

Jedwali Na 9: Miradi Mingine Inayotekelezwa na Halmashauri.  


NA
HALMASHAURI
AINA YA MRADI
KIASI CHA FEDHA CHA MRADI

1

SONGEA MC

Ujenzi wa Madarasa

227,250,000

Ukamilishaji wa mabweni 2

60,000,000

Ununuzi wa vifaa tiba katika zahanati

50,000,000

Ununuzi wa vifaa tiba katika vituo vya afya

150,000,000

Ukamilishaji wa ujenzi wa zahanati 1

50,000,000

Ujenzi wa hospitali ya wilaya awamu ya pili

500,000,000

JUMLA

1,037,250,000

2

TUNDURU DC

Mfuko wa Jimbo

135,950,000.00

Ukarabati wa hospitali kongwe za halmashauri

900,000,000.00

Fedha za mitihani darasa la nne (SFNA 2022)

261,518,000.00

Fedha za Mitihani ya darasa la saba (PSLEE 2022)

120,042,000.00

fedha za mitihani kidato cha pili (FTNA 2022)

179,645,000.00

Fedha za Mitihani Kidato cha nne (CSEE 2022)

261,518,000.00

Elimu bure Shule za Msingi (EMBM)

335,913,531.39

Elimu bure shule za Sekondari (EMBM)

475,995,800.00

Tozo ya upandaji miti

44,012,084.50

Ununuzi wa vifaa tiba kwa zahanati

100,000,000.00

Ukamilishaji wa zahanati

200,000,000.00

Ununuzi wa vifaa tiba kwa vituo vya afya

300,000,000.00

Ujenzi wa madarasa shule kongwe za Msingi

100,000,000.00

Ukamilishaji wa madarasa msingi

100,000,000.00

Mfuko wa Jimbo

135,950,000.00

TASAF

1,778,703,691.00

UNICEF CHANJO

39,565,250.00

JUMLA
5,468,813,356.89

3

MBINGA DC

EP4R

160,000,000

JUMLA

160,000,000.00

4

SONGEA DC

 Umaliziaji wa ujenzi wa zahanati za Magima na Mtimira B

100,000,000

Fedha za kuchochea miradi ya maendeleo (CDCF)

75,205,000

Ujenzi wa shule mpya ya Msingi lizaboni

250,000,000

Ukarabati shule ya msingi Liweta

100,000,000

Ujenzi Stand ya Mabasi kijiji cha parangu

225,145,486.29

Ujenzi nyumba ya Mtumishi na Kisima cha maji Zahanati ya mdunduwalo

170,995,797.32

JUMLA

921,346,283.61

5
NYASA DC
MAJENGO YA UTAWALA YANAYOENDELEA

448,402,504.81

6

MADABA DC

Ukamilishaji wa Ujenzi wa Bwalo Shule Ya Sekondari Wino

50,000,000.00

Ukamilishaji wa Ujenzi Wa Bweni Shule Ya Sekondari Matetereka

80,000,000.00

Ujenzi wa Nyumba 4 za Walimu Shule Za Msingi (Mtazamo, Igawisenga, Madaba, Kifaguro)

200,000,000.00

Ukamilishaji wa Ujenzi wa Zahanati ya Mahanje

50,000,000.00

Ukamilishaji Wa Maabara 3 Katika Shule Za Sekondari (Madaba, Lilondo, Matetereka)

90,000,000.00

Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya

750,000,000.00

Ukamilishaji wa darasa 1 shule ya msingi Mbangamawe

18,750,000.00

 

 

JUMLA

1,238,750,000.00

7
MBINGA TC
0

0

8
NAMTUMBO DC
0

0

JUMLA 
 
18,100,721,785.81


5.2.7 Baadhi ya Mafanikio ya utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya mwaka wa Fedha 2022/20223 kuishia Novemba, 2022

  • Kukamilisha kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa 35 ya kidato cha kwanza mwaka 2023 kati ya vyumba 156 vinavyotakiwa kujengwa.
  1. Kufanyika kwa vikao mbalimbali vya kisheria
  2. Kuendelea kulipa stahiki mbalimbali za watumishi
  3. Kuendelea na ujenzi wa jengo la ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Nyasa na Mbinga
  4. Kuanza maandalizi ya ujenzi wa Nyumba ya Katibu Tawala Mkoa, Nyumba ya Mkuu wa Wilaya Mbinga na Ofisi mbili (2) za Maafisa Tarafa.
  5. Maandalizi ya Mashamba Darasa nane (8) ya Malisho na Mashamba darasa matatu (3) ya kuku.
  6. Kuendelea kutoa mafunzo kwa vyama vya ushirika
  7. Ufuatiliaji na usimamizi wa Miradi ya maendeleo ya Kilimo cha Mazao ya chakula na mazao ya biashara
  8. Kuendelea na ujenzi wa soko la samaki katika mji wa Mbamba bay

5.2.8 Changamoto za utekelezaji wa Mpango na Bajeti wa mwaka 2022/2023.

  • Kupanda kwa bei ya vifaa vya ujenzi, bidhaa nyinginezo na huduma huduma mbalimbali, hivyo kuathiri utekelezaji wa shughuli zilizopangwa.
  1. Fedha za miradi ya elimu na afya kutolewa kwa viwango sawa nchi nzima (flat rates) bila kuzingatia umbali na tofauti za kijiografia za Mikoa, wilaya na Halmashauri. (Darasa mil.20 & 12.5, bweni mil.80 &100, nyumba mil.90 nk)
  • Ukubwa wa eneo la Mkoa wa Ruvuma (Kilomita za mraba 67,372) na umbali uliopo kati ya Makao Makuu ya Mkoa na Wilaya, hivyo kuongeza gharama za uendeshaji ukilinganisha na fedha zinazotolewa;
  • Upungufu na uchakavu wa magari katika Sekretarieti ya Mkoa na Halmashauri;
  • Upungufu wa watumishi katika Idara mbalimbali hususani katika Idara ya ujenzi, afya, elimu, kilimo, mifugo, fedha na Wathamini.

5.2.9 Mikakati ya Kutatua Changamoto

Kununua vifaa vya ujenzi moja kwa moja viwandani ili kupata unafuu wa bei

Kupunguza matumizi yasiyo ya lazima 

Kuendelea kuiomba Serikali kuridhia maombi ya kugawa maeneo ya kiutawala hususani Wilaya ya Tunduru pamoja na kuongeza fedha za uendeshaji wa shughuli za Mkoa na Halmashauri;

Kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa magari mapya na kufanya matengenezo ya magari yaliyopo.

Kuendelea kuwasilisha maombi ya vibali vya ajira ili kuongeza idadi ya watumishi na kuborehsa utoaji wa huduma mbalimbali.

5.3. Taarifa ya Maandalizi ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 

Mkoa umeanza maandalizi ya mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kwa kuainisha vipaumbele mbalimbali vya kisekta kwa kuzingatia nyaraka na miongozo mbalimbali iliyopo ya kimkoa na kitaifa ili kuhakikisha Mpango na Bajeti ya Mkoa unaendana na vipaumbele vya kitaifa vilivyoainishwa katika Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 - 2025/26, Mpango wa II wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2021- 2025, Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030 nk.

Sambamba na miongozo hiyo, Mpango na bajeti ya 2023/2024 utazingatia mwongozo wa Mpango na bajeti ya mwaka 2023/2024 uliotolewa na Wizara ya Fedha na Mipango ambao unaainisha na kutoa maelekezo mahususi yanayopaswa kuzingatiwa na Wizara, Mashirika, Taasisi za Umma, Wakala za Serikali, Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa wakati wa uandaaji wa Mipango na bajeti. Pamoja na kuzingatia vipaumbele vya Mwongozo wa mpango na bajeti, pia Mkoa utazingatia Vipaumbele vya Mkoa kama vilivyoainishwa katika Mpango Mkakati wa Mkoa wa miaka mitano (5) kuanzia 2021/2022 hadi 2025/2026, Mipango Mikakati ya Mamlaka za Serikali za Mitaa na Taasisi za Umma.

Baadhi ya Vipaumbele vya Mpango na Bajeti ya 2023/2024 ni kama ilivyoainishwa kwenye jedwali namba 10..

 

Jedwali Na 10: Vipaumbele vya Mkoa na Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2023/24

 

NA

SEKTA

VIPAUMBELE

1.
Utawala na Rasilimali Watu
Kuendelea kusimamia na kudumisha masuala ya ulinzi na usalama ndani ya Mkoa pamoja na usimamizi wa mipaka kwa kuratibu vikao vya ujirani mwema.
  • Kuimarisha utawala bora kupitia uratibu na uendeshaji wa vikao vya kisheria, kiutawala, uboreshaji wa Serikali mtandao na ushirikishwaji wa wananchi na ugatuaji wa madaraka kwa Umma (D by D);
Kuratibu na kusimamia utekelezaji wa Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa na Mpango Kazi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWA)
Kuboresha mazingira ya kufanyia kazi kwa kutenga fedha kwa ajili kujenga,kukamilisha na kukarabati nyumba na Ofisi za wakuu wa Wilaya,Wakurugenzi wa Halmashauri,Tarafa, Kata na Vijiji na nyumba za watumishi kwa kuweka kipaumbele katika maeneo ambayo hayana ofisi na nyumba za viongozi na watumishi;
2
Afya na Ustawi wa Jamii
Kuendelea kuboresha huduma za afya kwa kujenga, kukamilisha na kukarabati vituo vya kutolea huduma za afya na kuviwekea vifaa tiba na dawa.
Kuboresha huduma za afya na lishe katika ngazi ya jamii na vituo vya huduma za afya kwa kutenga bajeti ya uratibu, usimamizi na kujenga uwezo kuhusu masuala ya lishe sambamba na kutenga katika bajeti shilingi 1,000 kwa kila mtoto mwenye umri wa chini ya miaka mitano kwa ajili ya huduma za lishe.
Kusimamia na kufuatilia ubora (Quality) na utoaji wa huduma za Afya
      katika Hospitali, Vituo vya Afya na Zahanati
Kuendelea kutoa elimu ya kupambana na na kuchukua tahadhari dhidi ya  magonjwa hatari ya kuambukiza ikiwemo ugonjwa wa Ebola, UVIKO 19, na Ukimwi.
Kuendelea kuhamasisha wananchi kujiunga na Mfuko wa Jamii ulioboreshwa (iCHF).
Kuwajengea uwezo watumishi wa Idara ya Afya katika vituo vya
      kutolea huduma za Afya katika Halmashauri.
3.
Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Kundelea kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia katika shule za msingi na sekondari kwa kujenga, kukamilisha na kukarabati miundombinu ya shule.
Kuendelea kutekeleza Mpango wa kutoa elimu bila malipo kwa shule za msingi na sekondari ili kuwawezesha vijana wenye sifa kuanza na kuendelea na masomo bila kikwazo;
Kuuwezesha mafunzo kazini kwa walimu katika ufundishaji wa mada mbalimbali.
Kuboresha ufundishaji wa masomo ya sayansi na ufundi kwa kusambaza vifaa vya kufundishia masomo ya sayansi na kujenga maabara na karakana za ufundi.
4
Kilimo na Mifugo
  • Kuendelea kuongeza uzalishaji na tija (production and productivity) kwa mazao ya chakula  na biashara ili kuongeza kiwango cha utoshelevu na ziada ya chakula.
  • Kuwawezesha wakulima, wafugaji na wavuvi wadogo kupata utaalam na mbinu bora za kilimo na ufugaji kwa watalam wa kilimo na wakulima, wafugaji na wavuvi wakubwa ambao wapo kwenye maeneo yao ili kukuza uwezo na kuendeleza kilimo cha kisasa, chenye tija na cha kibiashara;
  • Kuendelea kusimamia upatikanaji na matumizi saahihi ya pembejeo na zana  bora za kilimo ili kuongeza tija katika uzalishaji;
  •  Kuanzisha Kongani za Kilimo na mazao ya Kilimo
  • Kuimarishaji usafiri na usafirishaji kwa kuendelea na Ujenzi wa barabara na madaraja, kukarabati na matengenezo ya barabara za Vijijini na Mijini kwa kuzingatia vipaumbele vilivyoainishwa kupitia Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2020,Mpango Mkakati wa Mkoa pamoja maeneo ya kimkakati ndani ya Mkoa (kilimo,madini, maeneo mapya ya makazi na huduma.
6
Nishati (Umeme)
Kuendelea na utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini na mijini inayotekelezwa na REA na TANESCO pamoja na kuendelea kuwaunganishia nishati ya umeme wananchi ili kuongeza kiwango cha upatikanaji wa umeme kwa ujumla (overall electricity access level)
7
Fedha na tehama 
Kuendelea kuimarisha na kusimamia Mifumo ya Kielektroniki ya Ukusanyaji wa Mapato (LGRIS),mifumo ya matumizi (MUSE,FFARS etc) ili kupunguza mianya ya upotevu wa mapato ya serikali sambamba na kuendelea kuhimiza matumizi ya mifumo ya malipo Serikalini (GePG).
Kuendelea kuongeza ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kubuni vyanzo vipya vya mapato na kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato katika vyanzo vilivyopo.
9
Uwezeshaji wa wananchi kiuchumi
Kuendelea kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia utoaji wa mikopo yenye mashariti nafuu inayotokana na 10% ya mapato ya ndani ya Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu (4:4:2).
Kuendelea kusimamia na kutekeleza Mpango wa Kunusuru kaya Masikini (Social Welfare Benefits) unaotekelezwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF II).
Kuendelea kutenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji mbalimbali kama viwanda, kilimo cha kimkakati, biashara nk.

Kwa kuzingatia ukomo wa bajeti  na vipaumbele vilivyoainishwa hapo juu, kwa mwaka wa fedha 2023/24 Mkoa wa Ruvuma fungu 82 unatarajia kuwasilisha maombi ya kuidhinishiwa jumla ya Shilingi 267,530,798,000.00 kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake. Fedha hizo zinajumuisha Shilingi.180,932,942,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Shilingi. 86,497,856,000.00 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi na Shughuli mbalimbali za maendeleo.

5.3.1 Matumizi ya Kawaida.

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma na  Halmashauri zake unatarajia kuwasilisha maombi ya  kuidhinishiwa jumla ya Shilingi.180,932,942,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Kati ya fedha hizo,Shilingi. 153,907,956,000.00 ni Mishahara ya watumishi na Shilingi. 27,024,986,000.00 ni Matumizi Mengineyo.  Aidha, bajeti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ni  Shilingi. 6,419,485,740.00 na Shilingi.174,513,456,260.00 ni kwa ajili ya Halmashauri.

5.3.2 Matumizi ya Maendeleo

Kwa mwaka wa fedha 2023/24, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Halmashauri zake  unatarajia kuwasilisha maombi ya  kuidhinishiwa makadirio ya jumla ya  Shilingi. 86,497,856,000.00 kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.  Kati ya fedha hizo, Shilingi. 34,172,550,000.00 ni fedha za ndani, Shilingi. 45,511,358,000.00 ni fedha za nje na Fedha za maendeleo mapato ya ndani ni Shilingi 6,813,948,000.00. Fedha maendeleo kwa ajili ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ni Shilingi. 2,285,721,000.00 na Halmashauri ni Shilingi. 84,212,135,000.00.

 

 

 

Matangazo

  • RATIBA ya Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 March 31, 2023
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara June 30, 2023
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma September 30, 2023
  • WALIOCHAGULIWA kidato cha kwanza March 31, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • BILIONI 20 za Rais Samia zilivyojenga shule mpya 11 na madarasa 656 Ruvuma

    March 26, 2023
  • RAIS SAMIA atoa zaidi ya shilingi bilioni 233 kutekeleza miradi Tunduru

    March 25, 2023
  • KAMATI ya Afya na Lishe Manispaa ya Songea ilivyodhamiria kuondoa utapiamlo na udumavu

    March 25, 2023
  • MFUKO wa Misitu Tanzania watos ruzuku ya miti kwa shule za Mbinga

    March 25, 2023
  • Tazama zote

Video

RAIS SAMIA alivyomaliza kero ya maji Songea
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 74 Songea

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: 0252602256

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.