• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

BALOZI Nchimbi awataka wanahabari kutumia kalamu zao vizuri

Imewekwa kuanzia tarehe: April 5th, 2025

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi, ametoa wito kwa wahariri na waandishi wa habari kuandika habari zinazojenga mshikamano katika taifa na sio zinazochochea chuki.

Ametoa wito huo wakati akifungua mkutano maalum wa jukwaa la wahariri Tanzania (TEF) uliofanyika katika ukumbi wa Kanisa Katoliki la Bombambili, uliopo manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

“Wahariri wa vyombo vya habari ambao ndio mnaruhusu habari yoyote itoke kwenye chombo cha habari, kama mngetumia nafasi zenu vibaya inawezekana nchi isingekuwa kama ilivyo leo, wahariri ndio chujio la habari zote katika taifa, kwa siku zote ambazo mmetimiza wajibu wenu mmefanya taifa letu kuwa na utangamano,” alisema Dkt. Nchimbi.

Dkt. Nchimbi ameeleza kuwa vyombo vya habari vinatakiwa kuhakikisha vinakemea wanasiasa wa upande wowote anayetamka mambo ambayo yanaweza kusababisha  vurugu au maumivu kwa raia na hata kupelekea vifo.

Pamoja na mambo mengine katika mkutano huo, amepongeza juhudi za Jukwaa la Wahariri kwa kuendesha uchaguzi wa viongozi wake kwa misingi ya demokrasia na uwajibikaji, akisema kuwa ni mfano mzuri wa taasisi zinazoendeshwa kwa uwazi na ushirikishwaji.

Naye Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, amesema wizara itaendelea kusimamia uhuru wa vyombo vya habari na maslahi ya wanahabari na wataendelea kushirikiana na wadau wa sekta hiyo ili kuhakikisha mazingiza bora ya uendeshaji wa vyombo vya habari nchini.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile, amezitaja changamoto ambazo zipo katika tansnia ya habari ambazo ni uendelevu wa kiuchumi, uhuru wa wanahabari pamoja na maslahi ya waandishi wa habari.

Hata hivyo amebainisha kuwa serikali inatambua changamoto hizo na imekuwa tayari kushirikiana na jukwaa hilo ili kuzitatua, na wanaamini kwamba kwa pamoja wanaweza kubuni mbinu bora za kuhakikisha vyombo vya habari vinabaki imara na kutoa huduma bora kwa jamii.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.