• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

BALOZI wa Msumbiji apongeza uboreshaji huduma hospitali ya Rufaa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: May 23rd, 2023

Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania Mheshimiwa Ricardo Mtumbuida  ameipongeza serikali ya awamu ya sita kwa kuboresha miundombinu katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma hali iliyosababisha hospitali hiyo kutoa huduma zenye viwango vya hospitali ya Rufaa.

Balozi Mtumbuida ametoa pongezi hizo katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Ruvuma,ambapo  ametembelea na kukagua baadhi ya majengo yakiwemo jengo la wagonjwa wa dharura(EMD),jengo la wagonjwa mahututi (ICU) Pamoja na majengo ya huduma nyingine zinazoendena na hospitali ya Rufaa ya Mkoa.

Awali akitoa taarifa ya hospitali hiyo Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma Daktari Bingwa Magafu Majura alisema hospitali hiyo ilianzishwa na wakoloni mwaka 1920 ambapo awali ilikuwa ni kambi ya jeshi la Waingereza.

Amesema mwaka 1946 serikali ya waingereza iliongeza majengo mengine kwa ajili ya kutoa huduma kwa wanajeshi na familia zao na kwamba ilipewa hadhi kuwa hospitali ya wilaya mwaka 1961 na kwamba mwaka 1964 ilipandishwa hadhi kuwa hospitali ya Mkoa wa Ruvuma.

Dr.Majura anabainisha zaidi kuwa hospitali hiyo ilipewa hadhi ya kuwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa mwaka 2009 ambapo amesema hospitali hiyo inatoa huduma zote muhimu ikiwa na vitanda 321 na  watumishi 431 wa kada mbalimbali wakiwemo madaktari bingwa wanane.

Ili kuboresha huduma za afya katika Hospitali hiyo, Dr.Majura amesema serikali imetoa shilingi milioni 630 kujenga jengo la dharura (EMD)  katika hospitali hiyo ambalo limeanza kutumika na kwamba serikali pia imetoa fedha kwa ajili ya wodi ya wagonjwa mahututi (ICU) yenye vitanda 12 ambayo tayari inatumika.

“Hospitali hii hivi sasa inatoa huduma mbalimbali kwa wagonjwa ndani ya Mkoa wa Ruvuma na baadhi ya wagonjwa wachache wanatoka nchi jirani ya Msumbiji’’,alisema Dr.Majura.

Akizungumza baada ya kukagua hospitali hiyo Balozi Mtumbuida amewapongeza madaktari na wauguzi wa hospitali hiyo kwa kazi nzuri wanayofanya ya kuwahudumia wagonjwa ambapo amesisitiza nchi ya Msumbiji wanatakiwa kufika katika hospitali hiyo kujifunza namna huduma bora za afya zinavyotolewa.

Akiwa Mkoani Ruvuma Balozi huyo ameweza kukutana na wananchi wa Msumbiji wanaoishi mkoani Ruvuma katika wilaya za Songea,Namtumbo na Tunduru ambapo amewasisitizia serikali ya Msumbiji  inafanya zoezi la usajiri wa wananchi wa Msumbiji wanaoishi nchini Tanzania hivyo wajitokeze ili kupata huduma muhimu wanazostahili kama raia wa Msumbiji.

Katika ziara hiyo Balozi huyo ametembelea Makumbusho ya Taifa ya Majimaji mjini Songea pia amekutana na uongozi wa Chama tawala CCM ngazi ya Mkoa wa Ruvuma.

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mheshimiwa Kapenjama Ndile amemweleza Balozi huyo kuwa ,serikali mkoani Ruvuma ipo tayari kuendeleza mahusiano mazuri na nchi ya Msumbiji  kwa kuendeleza ujirani mwema na jimbo la Lichinga nchini Msumbiji ambalo linapakana na wilaya ya Songea.

“Serikali mkoani Ruvuma inahimiza ujirani mwema na uhusiano mzuri baina ya Tanzania na Msumbiji kwa kuwa uhusiano huu umejengwa waasisi wa mataifa haya Mwl.Julius Nyerere na Samora Machel’’,alisisitiza Mheshimiwa Ndile.

Akizungumza kabla ya kuhitimisha ziara hiyo,Balozi huyo amesema wamefurahishwa na maendeleo makubwa yaliyofanyika katika Mkoa wa Ruvuma ikiwemo ujenzi wa miundombonu ya barabara za lami na miundombinu katika sekta za afya na elimu.

“Tanzania na Msumbiji sio nchi jirani tu bali ni ndugu wa historia ya damu kwa sababu mashujaa wengi wa Tanzania walipoteza Maisha nchini  Msumbiji,pia kuna wanajeshi wa Msumbiji waliopoteza Maisha yao huku Tanzania’’,alisisitiza.

Balozi huyo ni Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania kwa miaka miwili sasa hivyo anafanya ziara ya kujitambulisha kwenye mikoa ambayo ilitoa msaada wa hali na mali wakati wa harakati za ukombozi wa nchi ya Msumbiji.

Mikoa ambayo Balozi huyo amejitambulisha hadi sasa ni Dodoma,Iringa,Mbeya,Morogoro,Ruvuma na anatarajia kukamilisha ziara hiyo mkoani Mtwara.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Ofisi ya Mkoa wa Ruvuma

Mei 23,2023

  

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.