• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

BIASHARA ya makaa ya mawe ilivyoshamiri Ruvuma,tani zaidi ya milioni moja zauzwa nje

Imewekwa kuanzia tarehe: January 11th, 2023


BIASHARA ya madini ya makaa ya mawe mkoani Ruvuma imeshamiri baada ya mauzo jumla ya makaa ya mawe ya  tani 450,675.32  ndani ya nchi na tani 1,060,699.05 ziliuzwa nje ya nchi katika kipindi cha Julai hadi Desemba 2022.

Uchimbaji na uuzaji wa makaa ya Mawe Mkoani Ruvuma ulianza mwaka 2011 kukiwa na Kampuni moja tu ambayo ni Tancoal Energy Ltd.

Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Hamis Kamando amesema,mwaka 2019 wadau wengi walijitokeza na kufanya uwekezaji katika shughuli za Makaa ya Mawe hali iliyosababisha kuongezeka kwa uzalishaji wa madini hayo kuanzia mwaka 2020.

Amesema uzalishaji wa Madini ya Makaa ya Mawe unatoa mchango mkubwa kwenye maduhuli yanayokusanywa na Tume ya Madini Mkoani Ruvuma.

“Katika kipindi cha hivi karibuni, Makaa ya Mawe yamekuwa yakihitajika sana ulimwenguni kama chanzo cha nishati na hivyo kuwa moja ya chanzo kikubwa cha mapato ya Serikali’’,alisema Mhandisi Kamando.

Ametolea mfano,Katika Mwaka wa fedha 2021/2022, Ofisi ya Madini Mkoa wa Ruvuma ilipangiwa kukusanya maduhuli ya serikali kiasi cha Shilingi bilioni 12.

Hata hivyo amesema hadi kufikia Juni 30,2022, Ofisi ya Madini Ruvuma ilikuwa imekusanya kiasi cha Shilingi zaidi ya  Bilioni 21,sawa na asilimia 179 ya lengo la Mwaka huo.

Mhandisi Kamando amesema,Katika Mwaka huu wa fedha 2022/2023, Ofisi ya Madini Ruvuma imepangiwa kukusanya  zaidi ya  Shilingi Bilioni 26 na kwamba hadi kufikia Desemba 31,2022,Ofisi ya Madini Ruvuma imefanikiwa kukusanya  zaidi ya shilingi bilioni 19 sawa na asilimia 75.25 ya lengo.

“Katika makusanyo yote hayo, zaidi ya asilimia  85 yamechangiwa na uzalishaji na uuzwaji wa makaa ya mawe. Madini haya huuzwa ndani ya nchi, nchi zinazotuzunguka,barani Ulaya na Asia kupitia bandari ya Mtwara na Dar es Salaam’’,alisema..

Amesema katika Mkoa wa Ruvuma,kuna jumla ya wachimbaji 14 wanaochimba Makaa ya Mawe na kwamba katika Mwaka wa fedha 2021/2022 kiasi cha Madini ya Makaa ya Mawe kilichouzwa ni jumla ya tani 639,482.55 ziliuzwa ndani ya nchi na tani 837,846.29 ziliuzwa nje ya nchi.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema Kwa kipindi cha hivi karibuni Mkoa wa Ruvuma umeweza kuvutia na kupata wawekezaji wengi waliowekeza kwenye shughuli zinazohusiana na madini ya Makaa ya Mawe kama Uchimbaji, Ununuzi, Usafirishaji na Uchenjuaji.

Amezitaja faida za madini ya makaa ya mawe mkoani Ruvuma kuwa ni,Kuongezeka kwa mapato ya Serikali,Kuongeza kipato kwa mtu mmoja mmoja na kupunguza utegemezi kutokana na ajira zilizopo katika uchimbaji wa Makaa ya Mawe.

Faida nyingine ni kuongeza fedha za kigeni nchini kutokana na madini hayo kuuzwa nchi za nje  na Kuongezeka kwa mapato ya Halmashauri yatokanayo na ushuru wa huduma unaotozwa kwenye madini yanayochimbwa.

Shughuli za utafiti na uchimbaji wa makaa ya mawe katika mkoa wa Ruvuma zinafanyika katika Wilaya ya Mbinga maeneo ya Mbalawala,Mbuyula,Paradiso,Ntunduwaro,Amanimakoro na Ngaka, katika Wilaya ya Songea katika maeneo ya Muhukuru, Mdunduwalo,Njuga na kikunja na Wilaya ya Nyasa maeneo ya Malini.

Waziri Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa hivi karibuni ametembelea na kukagua mgodi wa makaa ya mawe wa Kampuni ya Jitegemee katika Kijiji cha Ntunduwaro wilayani Mbinga ambapo ameridhishwa kwa kushamiri kwa biashara hiyo.

Waziri Mkuu alifurahishwa na biashara ya makaa ya mawe baada ya kutembelea mgodi mmoja tu wa Jitegemee ambapo alielezwa mgodi umetoa ajira za kudumu 85,ajira za muda 150 ambapo alisema hiyo ni faida kubwa kwa wananchi na serikali ambayo inapata mapato makubwa kutokana na kodi na tozo mbalimbali.

Mkoa wa Ruvuma una hazina ya makaa ya mawe zaidi ya tani milioni 227 ambayo yanatarajiwa kuchimbwa kwa miaka 300.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Mkoa wa Ruvuma

Januari 11,2023

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.