• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

BILIONI 2.5 kumaliza kero ya maji Ngumbo Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: May 14th, 2023

KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 Abdalla Shaibu Kaim,ameweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji wa Ngumbo Group wilayani Nyasa unaotekelezwa na wakala wa maji safi na usafi wa mazingira vijijini(Ruwasa)kwa gharama ya Sh.bilioni 2,567,331,900.

Akitoa taarifa ya ujenzi Meneja wa Ruwasa wilayani Nyasa Mhandisi Masoud Samila alisema,mradi huo ulianza kutekelezwa rasmi mwezi  Septemba 2022 baada ya taratibu za manunuzi ya Mkandarasi kukamilika na ulitarajia kukamilika mwezi Machi 2023.

Alibainisha kuwa,hata hivyo kutokana na changamoto ya mvua zilizokuwa zikinyesha kwa wingi wilayani humo Serikali ililazimika kumuongezea muda wa utekelezaji ambapo kazi hiyo itakamilika Juni 2023.

Kwa mujibu wa Samila,mradi huo utakapakamilika utakuwa  na uwezo wa kuhudumia  zaidi ya wananchi 11,080  wa kijiji cha Ngumbo kwa awamu ya kwanza na ya pili ambao wanatembea umbali mrefu kutafuta huduma ya maji.

Samila alitaja kazi zilizofanyika ni ujenzi wa mtego wa maji(Intake),matenki mawili ya kutunzia maji yenye ujazo wa lita 75,000 na tenki la lita 200,000,mtandao wa bomba kuu na bomba la kusambaza maji lenye urefu wa kilomita 23.18  pamoja na vituo 12 vya kuchotea maji.

Alisema,hadi sasa utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 90 na Mkandarasi kampuni ya Nipo Africa Engineering Co Ltd ameshalipwa kiasi cha Sh.milioni 385,099,785,00 ikiwa ni malipo ya awali kati ya Sh.bilioni 2,567,331,900.

Kwa upande wake Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2023 Abdalla Shaibu Kaim,ameipongeza serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kutafuta majawabu ya changamoto zinazowakabili wananchi wake.

Alisema,mradi wa maji wa Ngumbo ni matokeo ya mapenzi makubwa ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa Watanzania na kuwataka wananchi kuendelea kuiunga mkono serikali yao.

Alisema,serikali imedhamiria kutekeleza kauli yake ya kumtua mama ndoo kichwani kwa kuhakikisha inaondoa na kumaliza kabisa changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini hususani maeneo ya vijijini.

“leo wananchi wa kijiji hiki na maeneo jirani tumeshuhudia namna serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mama yetu Dkt Samia Suluhu Hassan inavyoendelea kuhakikisha suala la upatikanaji wa maji linakwenda kumalizika katika maeneo yetu”alisema.

Amewataka wakazi wa Ngumbo, kuisaidia serikali kwa kuwa walinzi wa miundombinu ili miradi inayojengwa katika maeneo yao iweze kudumu kwa muda mrefu na kuwanufaisha vizazi na vizazi.

Amewaomba kutumia fursa hiyo kuvuta maji kwenye nyumba zao kwani kufanya hivyo itapunguza msongamano wa watu kwenye vituo vya kuchotea maji(DPS) na hivyo kurahisisha suala la upatikanaji wa huduma hiyo ya maji kwenye kaya zao.

Mbunge wa Jimbo la Nyasa Mhandisi Stella Manyanya,ameishukuru serikali ya awamu ya sita kupitia Wakala wa maji safi na usafi wa mazingira vijijini(Ruwasa),kwa kuendelea kutekeleza miradi ya maji maeneo ya vijijini na kupunguza adha ya upatikanaji wa huduma hiyo kwa wananchi

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.