• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

BILIONI 37 zilivyokamilisha ukarabati wa kiwanja cha ndege Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: February 25th, 2022

SERIKALI kupitia wakala wa Barabara nchini(Tanroad) imetumia Sh.bilioni 37,090,185,911.00 kufanya upanuzi na ukarabati wa kiwanja cha ndege kilichopo katika eneo la Ruhuwiko Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma , kilichoanza kufanyiwa upanuzi tangu Mwezi April 2019.

Hayo yamesemwa na Kaimu Meneja wa Tanroad mkoa wa Ruvuma Mhandisi Ephatar Mlavi,wakati akizungumzia ujenzi wa uwanja huo ambapo alisema hadi sasa kazi hiyo imekamilika kwa asilimia tisini.

Mlavi alisema,kazi zilizofanywa na Mkandarasi kampuni ya Chico katika mradi huo ni kujenga barabara ya kutua na kuruka ndege,kujenga ofisi ya Mhandisi mshauri ambayo baada ya kazi kuisha itakuwa jengo la muda la abiria,kujenga maegesho ya ndege na jengo la kuweka jenereta(Power House) kazi ambazo zimeshakamilika na uwanja umeanza kutumika.

Alisema,Mkandarasi ameshalipwa jumla ya Sh.19,555,560,906.98 kwa kuwa mradi ulikamilika tangu Mei 2021 na sasa upo kwenye muda wa matazamio ambapo Mkandarasi anaendelea na kazi ndogo ndogo.

Mhandisi Mlavi alitaja kazi zilizobaki na ambazo zinazoendelea kufanyika, ni kujenga jengo la kuongozea ndege(Control Tower)ufungaji wa taa,ufungaji wa mifumo ya umeme,mifumo ya mawasiliano na ununuzi wa gari la zimamoto.

Kwa upande wake Meneja wa kiwanja cha ndege cha Songea Jordan Mchami alisema baada ya matengenezo hayo uwanja huo kwa sasa una uwezo wa kutua ndege mbalimbali ikiwamo Bombadier.


Alisema, tangu kupunuliwa kwa uwanja huo kumefungua fursa ya kiuchumi kwa wakazi wa mkoa wa Ruvuma ambapo idadi ya abiria wanatumia usafiri wa ndege imeongezeka kufuatia kupungua kwa nauli ikilinganisha kabla ya upanuzi wa uwanja huo.
Aidha Mchami, ameiomba Serikali kujenga jengo la abiria kwani lililopo ni dogo linalotosheleza kukaa abiria 50 ikilinganisha na idadi ya watu wanaofika katika kiwanja hicho kwa ajili ya kusafiri.
Amewahimiza wakazi wa mkoa huo na mikoa jirani kuendelea kutumia usafiri wa ndege ambao ni rahisi kuliko usafiri wa basi katika kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi na kuyaomba mashirika mengine kuleta ndege zao mkoani Ruvuma kwani kiwanja hicho kimekamilika na kina uwezo wa kupokea ndege aina yoyote.

Mmoja wa mkazi wa Ruhuwiko Manispaa ya Songea Jeremiha Malon, ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kuleta mradi wa upanuzi wa kiwanja cha ndege kwani umesaidia sana kuleta ajira.

Pia alisema,kuletwa kwa mradi huo kumepunguza vitendo vya uharifu hasa kwa vijana wa Songea na kuongeza idadi ya watalii wanaofika kutembelea Hifadi ya Taifa ya Nyerere na kuwaomba wananchi wa mkoa wa Ruvuma na mikoa mingine jirani ya Mtwara,Njombe kutumia kiwanja hicho kwa kusafiri kwenda maeneo mbalimbali hapa nchini.

Hata hivyo,amemuomba mkandarasi aliyepewa kazi ya upanuzi wa kiwanja hicho kukamilisha kazi zilizobaki ikiwemo kufunga taa ili kiwanja hicho kiweze kutumika hata nyakati za usiku.
MWISHO.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.