• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

Councils directed to set Budget for Disabled-Deputy Minister Ikupa

Imewekwa kuanzia tarehe: February 22nd, 2018

HALMASHAURI NCHINI TENGENI BAJETI KWA AJILI YA WALEMAVU-NAIBU WAZIRI IKUPA

Songea                                                                                                                     

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye ulemavu Stella Ikupa ameziagiza halmashauri nchini kutenga fedha kwenye bajeti kwa ajili ya kuwezesha shughuli za watu wenye ulemavu.

Agizo hili amelitoa leo mjini Songea wakati alipoongea na viongozi wa mkoa wa Ruvuma na halmashauri ya manispaa ya Songea  akiwa kwenye ziara ya kukagua shughuli za watu wenye ulemavu.

Naibu waziri ameeleza kuwa tayari serikali ilikwisha agiza halmashauri zote kuwashirikisha watu wenye  ulemavu katika kujua mahitaji yao kwa serikali,hivyo ni muhimu kutenga bajeti katika mwaka 2018/19

Akitoa  taarifa ya mkoa kwa naibu waziri Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Joel Mbewa alisema tayari halmashauri zote za Ruvuma zimetekeleza agizo la serikali kwa kutenga asilimia ya mapato ya ndani  kwa ajili ya shughuli za walemavu mwaka ujao wa fedha

“Kwenye bajeti tunayoendelea kuandaa 2018/2019 mkoa wa Ruvuma umetenga asilimia kumi(10) ya mapato ya ndani kwa makundi  wanawake asilimia 4,vijana asilimia 4 na walemavu asilimia 2 “ alieleza Mbewa.

Naibu waziri alipongeza na kusisitiza kuwa fedha hizi baada ya Bunge kupitisha halmashauri zihakikishe zinawafikia walengwa na kutumika kwa miradi lengwa ili ziwanufaishe walemavu wote.

“Fedha zilizotengwa kwa kundi la walemavu lazima ziratibiwe vema na kuwanufaisha wengi.Walengwa waelimishwe kuwa fedha hizi lazima zirudishwe ili wengine pia wanufaike “ alisema Ikupa

Kwa mujibu wa takwimu za Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)  mkoa wa Ruvuma  kwa mwaka 2017 unakadiliwa  kuwa na watu  wapatao 1,542,296  ambapo watu wenye ulemavu wapo 12,972.

Taarifa ya mkoa inaonyesha mchanganuo  wa wenye ulemavu  na idadi yao kwenye mabano nikama ifuatavyo ; albino( 416),walemavu wa viungo (7,419),viziwi (1,527),wasioona (1,437),walemavu wa akili (1,907) na walemavu mchanganyiko (266).

Katika hatua  nyingine Naibu Waziri amemwagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Tina Sekambo kuacha kununua mafuta maalum kwa watu wenye ualbino kwa gharama kubwa ya shilingi 33,000 badala yake atafute yenye unafuu ili wahitaji wengi wanufaike na huduma hii.

Mkurugenzi huyo wa Manispaa alimweleza Naibu waziri kuwa katika mwaka huu wa fedha unaoishia Juni 2018 walitenga shilingi milioni moja na nusu kwa ajili ya kununua mafuta ya wenye ualbino lakini changamoto imekuwa gharama kubwa kwenye maduka ya mjini Songea hivyo imeleta kero kwa wahitaji.

“Nia ya serikali ya awamu ya tano ni kuwafikia  albino wengi  kwa kuwapatia mahitaji muhimu kwa gharama nafuu .Tafuteni mafuta haya kwenye maduka nje ya Songea kwa bei nafuu ili kuokoa fedha ya serikali” alisema Naibu waziri Ikupa

Naibu Waziri Ikupa amemuomba mkuu wa wilaya ya Songea Pololet Mgema kuhakikisha kunakuwepo mkakati maalum wa kuwatambua na kuwaandikisha watoto wote wenye ulemavu shuleni.

Alitoa wito huu kufuatia taarifa ya halmashauri kuonyesha katika mwaka huu ni watoto 164 pekee wenye ulemavu wameandikishwa kujiunga na darasa la kwanza kwenye kata nane kati ya ishirini na moja za Manispaa hiyo

Naibu waziri  Ikupa alisema”tunataka kila mtoto mwenye ulemavu atambuliwe na kupata haki yake ya msingi ya elimu” hivyo watumieni wenyeviti wa mitaa na vijiji kujua kaya zote zenye watoto wenye ulemavu ambao hawajapelekwa shuleni hadi sasa.

Mwisho.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.