• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

DC NAMTUMBO awaasa CWT kuchagua viongozi wenye maadili

Imewekwa kuanzia tarehe: March 22nd, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, mkoani Ruvuma, Mhe. Ngollo Malenya, amewataka wanachama wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kuchagua viongozi makini na waadilifu badala ya wanaharakati katika uchaguzi wa viongozi wa chama hicho kwa kipindi cha mwaka 2025 hadi 2030.


Alisema kuwa uongozi bora ni msingi wa maendeleo ya walimu na sekta ya elimu kwa ujumla.

Akizungumza lwakati wa Mkutano Mkuu wa CWT wilayani Namtumbo, uliofanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari ya wasichana ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mhe. Malenya alisisitiza umuhimu wa viongozi wenye maadili, uwajibikaji, na ushirikiano mzuri na serikali.

Alisema viongozi hao wanapaswa kuwa tayari kushirikiana na serikali ili kutatua changamoto za walimu kwa njia ya busara na mazungumzo yenye tija.

“Ni muhimu kuchagua viongozi, si wanaharakati. Tunahitaji watu watakaoshirikiana na serikali kuhakikisha walimu wanapata haki zao kwa njia ya busara, hekima, na mazungumzo yenye tija,” alieleza Mhe. Malenya.

Mhe. Malenya pia alisisitiza umuhimu wa walimu na viongozi wao kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi zake za kuboresha sekta ya elimu.

Alisema kuwa serikali imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika elimu, hivyo ni jukumu la walimu kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii, maarifa, na uzalendo ili kufanikisha azma hiyo.

Mkutano huo ulikuwa ni sehemu ya maandalizi ya uchaguzi wa viongozi wa CWT wilayani Namtumbo kwa kipindi cha mwaka 2025 hadi 2030. Ulijumuisha walimu kutoka shule mbalimbali za msingi na sekondari,.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.