• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

DC NAMTUMBO awafunda walimu

Imewekwa kuanzia tarehe: March 20th, 2023

MKUU wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma  Mheshimiwa  Ngollo Ng’waniduhu Malenya  amewataka walimu wilayani  Namtumbo  kusimamia maadili katika shule zao ili kudhibiti mmomonyoko wa maadili ambao unajitokeza hivi sasa.

Mheshimiwa Malenya aliyasema hayo kwenye kikao kilichowashirikisha waratibu elimu kata,walimu wakuu,maafisa idara ya elimu,afisa tume ya utumishi wa walimu( TSC) na afisa kutoka ofisi ya mkaguzi na mdhibiti ubora wa  shule.

Aidha Malenya  amesema mmomonyoko wa maadili hivi sasa unazidi kuongezeka na kuwataka walimu hao kusimamia kudhibiti umomonyoko wa maadili  kwa kutoruhusu kufanyika mapenzi mashuleni kati ya walimu  wa kiume na wanafunzi wa kike  lakini pia walimu wa kike na wanafunzi  wa kiume,lakini pia wanafunzi kwa wanafunzi .

Hata hivyo Malenya  alifafanua kuwa yeye ni mpenda mabadiliko yaliyochanya ,mpenda ukweli  na mpenda  usafi ,na kuwaomba walimu na viongozi wote wa wilaya ya Namtumbo kufanyakazi kama timu kwa kushirikiana kwa dhati ili kuwa na taswira ya ushindi katika mambo yanayofanyika wilayani humo.

Lakini pia mkuu wa wilaya huyo aliahidi walimu  kwenda kuzungumza na wananchi kila kata wilayani humo kuhimiza swala la wanafunzi  kupata chakula shuleni ili kuwasaidia wanafunzi hao waweze kujikita zaidi katika masomo badala ya kutembea umbali mrefu kufuata chakula na wakati mwingine kutopata chakula kabisa.

Mkurugenzi  wa Halmashauri  ya wilaya ya Namtumbo Chiriku Hamis Chilumba  pamoja na mambo mengine alimwambia mkuu wa wilaya kuwa halmashauri ya wilaya ya Namtumbo ina jumla ya walimu 882 huku mahitaji ni walimu 1351 ambapo sasa kuna upungufu wa walimu 469 .

Afisa elimu Msingi wa Halmashauri ya  wilaya ya Namtumbo  Juma Fulluge aliagiza walimu wakuu kusimamia taaluma mashuleni  kwa kuhakikisha walimu wanafundisha ipasavyo na  kwa kumaliza mada zilizopo .

Fulluge  alisisitiza kuwa  ofisi yake itakuwa inafuatilia ufundishaji katika kila shule,ufanyikaji wa mitihani ya mihula,ufanyikaji wa majaribio ya kila mwezi  na utoaji wa mazoezi  kwa wanafunzi  na kukazia  ufundishaji kwa vipindi vya ziada kwa wanafunzi wa darasa la nne na la saba.

Mustapha  Ponera mwalimu mkuu wa shule ya msingi Namtumbo akizungumza kwa niaba ya walimu wakuu wenzake alisema wao kama walimu wakuu wanaenda kusimamia taaluma ipasavyo na kuwahakikishia viongozi wa wilaya ya Namtumbo  kuwa yale yote yaliyosisitizwa na viongozi hao yanaenda kufanyiwa kazi  na matokeo chanya yatapatikana alisema mwalimu huyo.

Kikao cha walimu wakuu,waratibu elimu kata na maafisa wilayani Namtumbo kilifanyika jana katika ukumbi wa Halmashauri ambapo lengo la kikao hicho kilikuwa kuwahimiza kusimamia majukumu yao ya kila siku kwa kuwasisitiza walimu kufundisha madarasani pamoja na ugawaji wa vishikwambi 21 kwa waratibu elimu kata  kwa kata21 zilizopo  wilayani Namtumbo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.