• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

DC NAMTUMBO awapongeza walimu kwa kusimimia utekelezaji wa miradi

Imewekwa kuanzia tarehe: March 27th, 2025

MKUU wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma, Ngolo Malenya, amewapongeza walimu wa wilaya hiyo kwa juhudi zao katika kusimamia na kutekeleza ujenzi wa miundombinu ya shule za msingi na sekondari.

 Akizungumza jana wakati wa kufungua mkutano mkuu wa uchaguzi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Wilaya ya Namtumbo uliofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Dkt. Samia Suluhu Hassan, Malenya alisisitiza kuwa walimu ni wadau muhimu wa maendeleo katika sekta ya elimu na jamii kwa ujumla.

Malenya alibainisha kuwa walimu siyo tu wanawajibika katika kuwajengea wanafunzi msingi mzuri wa elimu, bali pia wanashiriki moja kwa moja katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayopelekwa kwenye shule zao. 

Hata hivyo, aliwataka walimu kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa weledi na kwamba Serikali haitasita kuwachukulia hatua wale watakaoshindwa kusimamia ujenzi wa miundombinu ya shule au kwenda kinyume na maadili ya kazi yao.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Wilaya aliwaagiza maafisa elimu wa shule za msingi na sekondari kuhakikisha wanazingatia sheria na taratibu wanapohamisha watumishi kutoka kituo kimoja cha kazi kwenda kingine. Alisisitiza kuwa ni muhimu kuhakikisha watumishi wanalipwa stahiki zao kikamilifu ili kuepusha usumbufu unaoweza kutokea.

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Walimu Wilaya ya Namtumbo, Deograsias Haule, alisema chama hicho kina wanachama 1,292 ambapo 1,265 kati yao sawa na asilimia 98 ni wanachama hai. Alieleza kuwa matarajio yao ni kuhakikisha walimu wote wanajiunga na chama hicho.

 Haule pia alimpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kupewa dhamana ya kupeperusha bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu ujao, akisisitiza kuwa walimu wanatambua juhudi za serikali katika kuboresha sekta ya elimu.

Katika uchaguzi wa chama hicho, Mwalimu Jacob Mbunda alichaguliwa kuwa mwenyekiti mpya baada ya kupata kura 66 na kumbwaga aliyekuwa mwenyekiti wa zamani, Anna Mbawala, aliyepata kura 35. Uchaguzi huo ni sehemu ya mchakato wa kuimarisha uongozi wa chama katika ngazi ya wilaya kwa miaka mitano ijayo.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.