• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

DC SONGEA aagiza watendaji wa Kata,Mitaa kusimamia mikataba ya lishe

Imewekwa kuanzia tarehe: April 18th, 2021

Mikoa ya nyanda za juu kusini,  utafitI unaonyesha ndiyo inayoongoza kuwa na kiwango kikubwa cha watoto wenye udumavu na utapiamlo.

Kauli hiyo imebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema akiwa katika kikao cha tathimini ya Lishe Manispaa ya Songea kilichohudhuriwa na maafisa wa Watendaji Kata 21 na wataalamu wa afya kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea jana tarehe 15 aprili 2021.

Pololet alisema lengo la kuweka tathimini katika kila robo moja ya mwaka  ni kuweka mkakati na mpango kazi wa lishe bora kwa jamii  ili kuhakikisha tunapunguza au kuondoa kabisa tatizo la watoto wenye udumavu na utapiamlo Mkoani   Ruvuma hasa Songea Mjini.

Aliongeza kuwa  nyenzo muhimu ya kutekeleza mkakati wa lishe Manispaa ya Songea ni kutoa elimu kwa jamii ili kuondoa changamoto zinazojitokeza za ongezeko la watoto wenye udumavu na utapiamlo kwa watoto walio chini ya miaka mitano 5  kutoka asilimia  0.08%  septemba 2020 hadi asilimia 0.16%   januari hadi machi ikiwa ni ongezeko kubwa kuliko kipindi cha nyuma.

Alisema ongezeko hilo linatokana baadhi ya akimama wajawazito kutohudhuria kliniki kwa wakati, wahudumu wa afya na watendaji wa kata na Mitaa  kutotembelea kaya zenye wajawazito na watoto walio chini ya miaka mitano 5,  ukosefu wa elimu  ya Lishe kwa Maafisa watendaji wa kata na Mitaa, pamoja na kukosekana kwa sheria ndogo ndogo za mkataba wa lishe kwa watoto walio chini ya miaka mitano 5.

Pololet amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa Songea Tina Sekambo kuwawezesha Maafisa wa watendaji wa kata kupata elimu ya mafunzo ya Lishe ili waweze kutoa elimu sahihi ya lishe kwa jamii, pamoja na uandaaji wa taarifa zenye takwimu sahihi, uwajibikaji wa kazi na uwazi wa utawala bora katika maeneo yao ya kazi  kwa  kubandika taarifa za kiutendaji katika mbao za matangazo pamoja na kuzingatia kanuni ya  uendeshaji wa vikao vya kisheria ifikapo kila robo moja ya mwaka na uandaaji wa sheria ndogo za lishe.” Alisisitiza” .

Naye Afisa Lishe Manispaa ya Songea Florentine Joseph Kissaka alisema jumla ya watoto wenye utapiamlo mkali waliopewa rufaa kwenda kwenye matibabu ni 29 ambao  walitoka kata za matarawe 1, misufini 1, matogoro 21, Ruhuwiko 1, na Msamala 5 kati ya watoto 17,840 waliopimwa sawa na asilimia 0.16  ya wenye utapiamlo katika kipindi cha januari-machi.

Kissaka alibainisha kuwa jumla ya vijiji vilivyofanya mkutano siku ya afya na lishe ni 91 kati vijiji 95 sawa na asilimia 95.8% ya  utekelezaji wa zoezi hilo. Aliongeza kuwa vijiji vyenye sheria ndogo za lishe ni 77 kati ya vijiji 95 sawa na asilimia 81.1%,  vijiji vilivyobandika taarifa ni 86 kati ya vijiji 95 sawa na 90.5%.

Miongoni mwa mikakati iliyowekwa ili kukabiliana na ongezeko la watoto wenye udumavu na utapiamlo Manispaa ya Songea ni pamoja na kuendelea  kutoa elimu  kwa jamii namna ya uandaaji wa chakula cha  lishe kwa mtoto chini ya miaka mitano, mpangilio wa ulaji wa chakula, na aina ya chakula kinachofaa kuliwa.

Imeandikwa na Amina Pilly

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.