• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

DC Songea ahimiza wazazi na walezi kuchangia chakula shuleni

Imewekwa kuanzia tarehe: May 19th, 2023

MKUU wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Kapenjama Ndile amewataka Watendaji wa Kata na Vijiji kwa kushirikiana na Walimu wakuu wa shule kuendelea kuhamasisha Wazazi juu ya uchangiaji wa chakula mashuleni.

Ameyasema hayo wakati wa kikao cha utekelezaji wa tathmini ya Afua na Mkataba wa Lishe kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano Lundusi- Peramiho na kuudhuriwa na kamati ya Lishe ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Aidha, DC Ndile katika kikao hicho amewasisitiza Watendaji wa Kata waje na mtizamo mpya wa kutoa taarifa za utekelezaji wa Afua za Lishe kwa uharaka na ziwe sahihi.

“Naendelea kuwasisitiza Watendaji jitahidini sana kuwahisha taarifa, jambo lingine nawaomba Maafisa Elimu muwahamasishe walimu wakuu kuongea na wazazi wa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ili waweze kuchangia chakula mashuleni na kuhakikisha kila mwanafunzi anapata chakula akiwa shuleni”, amesema DC Ndile.

Akizungumza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Ndugu Neema Maghembe amesema katika kipindi cha robo ya tatu mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri imefanya shughuli za usimamizi elekezi ambazo ni kuangalia utoaji wa Elimu ya Lishe katika Vituo vya kutolea Huduma za Afya, Utambuzi na matibabu ya Utapiamlo mkali na upimaji wa hali ya Lishe kwa Watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

“Sisi Halmashauri ya Wilaya ya Songea katika kutii agizo la Serikali la kutekeleza Afua za Lishe tumekuwa na mwelekeo chanya wa kutoa fedha za kutekeleza shughuli za Lishe kwa wakati ili kuhakikisha shughuli hizi zinaenda vizuri”, amesema Ndugu Neema.

Akisoma taarifa ya utekelezaji Afisa Lishe Wilaya Joyce Kamanga amesema katika robo ya tatu Watoto waliogundulika na Utapiamlo mkali walikuwa 18 kati ya hao Watoto wote wamepona baada ya kupatiwa matibabu.

Vilevile amesema Halmashauri imejipanga vizuri katika suala la kuimarisha usimamizi, pia katika kushirikisha kamati za Kata na Vijiji na wataalamu walioko katika ngazi ya Kata kwenye suala zima la kusimamia maadhimisho ya siku ya afya na lishe ambapo Wataalamu wanatoa Elimu kwa wazazi juu ya maandalizi ya Lishe na Watoto wanapata nafasi ya kupima hali ya Lishe katika Vijiji.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.