• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Madaba yaongoza elimu ya sekondari miaka mitatu mfululizo

Imewekwa kuanzia tarehe: April 13th, 2021

HALMASHAURI ya Wilaya ya Madaba  wilayani Songea mkoani Ruvuma,imefanya tathimini ya maendeleo ya  Elimu na kufanya vizuri miaka mitatu mfululizo kuanzia mwaka  2018 hadi 2020 katika matokeo ya elimu ya sekondari mkoani Ruvuma.

Akifungua kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololeti Mgema amesema katika Halmashauri zote nane zilizopo mkoani Ruvuma,Halmashauri ya Madaba imeshika nafasi ya kwanza katika mtihani wa kidato cha nne na kwamba  Mkutano huo wa tathmini umelenga kuongeza mikakati ya kufanikiwa zaidi katika sekta ya Elimu.

“Tunapozungumzia tathmini ya Elimu tunawagusa moja kwa moja walimu,maswala mengine tunapoona tumekwama  moja kwa moja hili swala linakuwa la walimu wametukwamisha na tukifanikiwa tunasahau kusema tumefanikiwa kwa sababu ya walimu  tunaomba mtuvumilie”.

Mkuu wa Wilaya amewaomba walimu kuwa huru kuzungumza changamoto zao mambo yaliyopelekea kufanya vizuri na yaliyokwamisha kutofa fanyika vizuri katika sekta ya Elimu.

Mgema ametoa rai kwa Madiwani wa Halmashauri hiyo kutoa changamoto zinazozikabili shule ambazo zipo kwenye kata zao ili ziwekewe mikakati ya kuzitatua hatimaye kufanya vizuri zaidi.

“Tunatambua uwepo wa wadau wengine kama mchango wa bank yaNMB katika Halmashauri ya Madaba wametuchangia kwa kiasi kikubwa katika sekta ya Elimu,pia TFS nao wametuchangia kwa kiasi kikubwa sana kama mabati,saruji tunaomba muendelee kusukuma gurudumu la Elimu katika halmashauri yetu ya Mdaba’’.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Shafi Kassim Mpenda katika kikao hicho amesema mbinu zinazotumika katika  kuhakikisha wanafunzi wanadhulia masomo yao vizuri na kufanya zizuri darasani  wameweka utaratibu wa kuwatumia watendaji,waratibu wa elimu kata katika ufuatiliaji.

Hata hivyo Mpenda amesema pia wameweka mkakati wakufanya mitihani ya muhula na nusu muhula na pale tu wanapofungua shule wanafanya mitihani iliyopelekea Halmashauri hiyo kufanya vizuri.

“ Tumeimarisha utawala bora shuleni tumekuwa na vikao vya mara kwa mara na walimu wakuu bodi za shule na vikao vya wazazi na kazi hiyo ni endelevu hata kwa walimu wanaokiuka tunawasikiliza kabla ya kuwachukulia hatua, na kuhakikisha walimu wanafanya kazi katika mazingira rafiki japo siyo rafiki kwa asilimia mia moja”.

Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Orap Pili amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kwa usimamizi  na walimu wote kwa kazi nzuri wanayofanya na kufikia kuongoza kwa miaka mitatu mfululizo na kupata heshima kubwa katika Halmashauri ya Madaba.

Aidha Makamu Mwenyekiti ameendelea kuwaomba walimu wa Halmashauri hiyo kuwa wavumilimu kutokana na changamoto zinazojitokeza katika mazingira magumu,kwa niaba ya Madiwani amewaahidi walimu kushirikiana  katika maeneo ya kazi katika kata na kufuatilia maazimia yaliyowekwa.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa habari Halmashauri ya Madaba

April 12,2021.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.