• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HALMASHAURI ya Madaba yapata hati safi miaka mitatu mfululizo

Imewekwa kuanzia tarehe: June 6th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ameipongeza Halmashauri ya Madaba wilayani Songea kwa kupata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo.

Mndeme ametoa pongezi hizo wakati anafungua kikao maalum cha Baraza la madiwani la Halmashauri hiyo cha kujadili taarifa ya hoja na mapendekezo ya CAG kwa mwaka 2018/2019 kilichofanyika kwenye ukumbi wa shule ya sekondari ya Madaba.

Taarifa ya CAG imeripoti kuwa Halmashauri ya Madaba imepata hati safi kuanzia mwaka wa fedha 2016/2017 hadi 2018/2019,ambapo Mndeme amesema kupata hati safi katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo ni jambo la la kutiliwa mfano.

Mkuu wa Mkoa pia ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kuchangia kwa asilimia 81.67 mfuko wa wanawake,vijana na wenye ulemavu kwa kuchangia shilingi milioni 32 katika bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019 na kukusanya zaidi ya shilingi milioni 578 sawa na asilimia 70.13.

Ili kuhakikisha kuwa Halmashauri hiyo inaendelea kupata hati safi,Mkuu wa Mkoa ameagiza kuzuia hoja za aina ile ile zinazojirudia mwaka hadi mwaka na wataalam kuendelea kutoa ushirikiano wakati wa ukaguzi.

“Hakikisheni mnadhibiti upotevu wa mapato katika Halmashauri na vyanzo vya mapato vidhibitiwe kwa kuchukua hatua stahiki,hakikisheni wanaodaiwa wote kupitia mashine za kukusanya mapato POS  wanalipa madeni yao mara moja’’,alisisitiza Mndeme.

Katika hatua nyingine Mndeme amewaagiza wataalamu wa afya katika Halmashauri hiyo, kuhamasisha wakulima kuongeza uzalishaji wa zao la tangawizi na kujenga viwanda vya kusindika zao hilo.

Utafiti umebaini kuwa Halmashauri ya Madaba ina eneo lenye ukubwa wa hekari 888 zinazofaa kwa kilimo cha tangawizi ambapo hadi sasa wakulima wanaolima zao la tangawizi ni 256 tu ambapo Mndeme  ameomba zao hilo lipewe kipaumbele kwa kuongeza kasi ya uzalishaji wake.

Mndeme ameshauri kuongeza kasi ya uzalishaji wa zao la tangawizi kutoka malengo ya uzalishaji wa zao hilo kwa mwaka 2019/2020 ya kuvuna tani 7511 kutoka hekari  288 ambapo amesema hayo ni malengo ya chini kwa kuwa soko la zao hilo ni kubwa ndani na nje ya nchi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Madaba Festus Mfikwa amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kutekeleza maagizo yote aliyotatoa ili Halmashauri  hiyo iendelee kupata hati safi kila mwaka na kuinua uchumi kwa kuongeza uzalishaji wa zao la tangawizi na mazao mengine kama mahindi na mapalachichi.

Mfikwa amesema Halmashauri ya Madaba inapata maendeleo kutokana na ushirikiano na umoja uliopo baina ya madiwani na watalaam.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Juni 6,2020

Madaba

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.