• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HEKARI moja ya mitiki inaweza kumuingizia mkulima milioni 400

Imewekwa kuanzia tarehe: July 13th, 2020

OFISA Maliasili wa Halmashauri ya Nyasa Mkoani Ruvuma Bugingo Bugingo amesema hekari moja ya miti ya mitiki inaweza kumuingizia mkulima zaidi ya milioni 400.

Bugingo amesema  Halmashauri ya Nyasa inatekeleza mradi wa panda miti kibiashara ikiwa imeweka lengo la Kupanda miti hekari  1750  ambapo hadi  sasa miti hekari 317.5 imepandwa na inaendelea vizuri.

Hata hivyo wakulima wengi mwambao mwa ziwa Nyasa wanakata tamaa ya kupanda miti hiyo ambayo tangu kupandwa hadi kuvunwa  inachukuwa kati ya miaka 15 hadi 20.

Mradi wa Pandamiti kibiashara unatekelezwa katika safu ya Milima ya Livingstone,Kata za Lipingo, Liuli, na Kihagara Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma unaendelea kwa kiwango cha kuridhisha.

Mratibu wa Mradi wa Forvac Mkoa wa Ruvuma Marcel Mtunda ,akikagua mradi wa panda miti kibiashara unaotekelezwa  katika kijiji cha Mkali A na Kijiji cha Nkalachi Kata ya Liuli,  ameridhishwa na maendeleo ya ukuaji wa miti, na kuwaomba wananchi wapalilie miti hiyo, ili isiungue na moto.

 Amesema  wananchi mara baada ya kupata elimu ya upandaji miti kibiashara, wamehamasika na kupanda miti ambapo amesema mradi huo utawanufaisha wakulima wa Miti katika vijiji hivyo kwa kuinua hali ya maisha na kuongeza kipato katika ngazi ya Familia.

Ben Mfungo ni Rais wa Shirikisho la Viwanda vya Misitu Tanzania (SHIVIMITA) tangu mwaka 1988,anabainisha mahitaji ya soko la miti aina ya mitiki ni kubwa ndani na nje ya nchi.

“Juzi tu nilikuwa Accra nchini Ghana ,tulijulishwa kwamba Jumuiya ya ECOWAS ilichukua mbegu za miti ya mitiki toka Tanzania baada ya kubainika mbegu za Tanzania zina ubora zaidi katika soko la dunia hivyo nao wameamua kuchukua mbegu hiyo inayokidhi soko la kimataifa’’,anasisitiza Mfungo.

Anawaasa wakulima wapya wa mitiki katika wilaya ya Nyasa na maeneo mengine ambayo zao hilo linaweza kustawi, waongeze uzalishaji wa zao la mitiki kwa sababu tangu enzi hizo hadi leo mahitaji yake yanaendelea kuongezeka.

Anayataja miongoni mwa matumizi ya zao la mitiki kuwa ni kutengenezea vitako vya silaha aina ya bunduki,vyombo vya majini kama vile meli na boti, na kwamba ujenzi wa mahakama kubwa duniani imetumika miti aina ya mitiki kwa sababu ndiyo mti mgumu ambao unaweza kuishi majini na nchi kavu,pia hutumika kutengeneza samani mbalimbali zenye gharama kubwa.

“Mahitaji ya mti huu katika soko la duniani ni makubwa ,ndiyo maana nchi za Ulaya na nchi za Asia zikiongozwa na China na India wananunua miti aina ya mitiki kwa wingi kutoka Tanzania,na hata hatujaweza kufikisha hata robo ya mahitaji yao’’,anasisitiza Mfungo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wiaya ya Nyasa Jimson Mhagama ametoa rai kwa wananchi, na kampuni za wawekezaji wanaohitaji kuwekeza  katika sekta ya Misitu  wafikie katika  Wilayani Nyasa kuwekeza  kwenye ardhi yenye rutuba ya kutosha .

Katika mkoa wa Ruvuma mradi huo uliofadhiliwa na nchi ya Finland unafanyika katika Halmashauri za Wilaya ya Nyasa,Mbinga na  Madaba wilayani Songea.

Mshauri wa Misitu katika Mradi wa Panda Miti Kibiashara Sangito Sumari anasema katika wilaya ya Nyasa mradi huu unahusu miti aina ya mitiki ambayo utafiti umebaini inastawi vizuri katika hali ya hewa iliyopo mwambao mwa ziwa Nyasa.

Imeandikwa na Albano midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Julai 13,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.