• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HOSPITALI ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea kuanza kutoa huduma Julai 15

Imewekwa kuanzia tarehe: July 7th, 2020

HOSPITALI ya Halmashauri ya Wilaya Songea mkoani Ruvuma ambayo imejengwa katika kijiji cha Mpitimbi B kwa gharama ya shilingi bilioni 1.8 inatarajia kuanza kutoa huduma za matibabu kuanzia Julai 15 mwaka huu.

Akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa hospitali hiyo kwa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma katika eneo  la mradi,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Simon Bulunganija amesema mradi huo umefikia asilimia 95 ya utekelezaji ambapo amezitaja huduma ambazo zitaanza kutolewa na hospitali hiyo ni za wagonjwa wa nje (OPD).

Amesema ujenzi wa hospitali hiyo ulianza mwaka 2019 na kwamba katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi huo Halmashauri ilipokea shilingi bilioni 1.5 ambazo zilijenga hadi katika hatua ya ukamilishaji.

“Nachukua fursa hii kwa niaba ya wananchi wa Halmashauri ya Songea  kumshukuru Rais Dkt.John Magufuli  kwa kutuongeza shilingi milioni 300 na kufanya mradi kutumia sh.bilioni 1.8 kutekeleza mradi huu’’,alisema Bulunganija.

Hata hivyo amesema hadi sasa zimetumika zaidi ya shilingi bilioni 1.5 na kwamba wanatarajia majengo yote saba ya hospitali hiyo kukamilika  Julai  30 mwaka huu na kuwezesha huduma zote za afya kuanza kutolewa katika hospitali hiyo.

Amesema hospitali hiyo inatarajia kuhudumia kata zote za Halmashauri ya Wila ya Songea ,hata hivyo amezitaja changamoto zilizopo katika mradi huo ni  mgawo wa maji ambao husababisha mafundi kukwama kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo kwa wakati.

Ameyataja majengo ya hospitali hiyo yanayoendelea kukamlishwa kuwa ni  jengo la utawala ambalo limefikia asilimia 90,jengo la wagonjwa  wa nje asilimia 80,stoo ya dawa asilimia 92,ujenzi wa maabara asilimia 92,jengo la vipimo vya mionzi asilimia 85,jengo la kufulia asilimia 90 na jengo la wazazi asilimia 90.

Akizungumza mara baada ya ukaguzi wa hospitali hiyo,Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho ameupongeza uongozi wa Halmashauri hiyo kwa kutekeleza mradi huo,hata hivyo amewaomba kuongeza kasi ili wananchi waanze kupata huduma hiyo.

“Sisi tunakimbizana na muda mwaka 2015 tuliwaahidi wananchi kwamba tutawasogezea huduma ya afya jirani hivyo tunataka wananchi waanze kupata huduma zote ili wakati wa Kampeni tuwaambie wananchi tuliahidi tumetekeleza’’,alisisitiza Mwisho.

Katika kukabiliana na changamoto ya upungufu wa maji,Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini RUWASA katika Wilaya ya Songea Mhandisi Samwel Sanya amesema wanatarajia kupeleka huduma ya maji katika hospitali hiyo ifikapo Julai 30 mwaka huu.

Naye Mbunge wa Jimbo la Peramiho Jenista Mhagama ameutaja mpango wa muda mrefu wa kukabiliana na upungufu wa  maji katika eneo la hospitali na wakazi wa kijiji cha Mpitimbi ni kuchimba visima virefu na kwamba fedha za kutekeleza mradi huo katika jimbo zima la Peramiho  zimekwishapokelewa.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Julai 7,2020

Songea

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.