• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HOSPITALI ya Nyasa kimbilio la watanzania na Msumbiji

Imewekwa kuanzia tarehe: February 18th, 2025

Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa  mkoani Ruvuma iliyojengwa eneo la Nangombo imeendelea kuwa tegemeo kubwa kwa wakazi wa wilaya na nchi jirani ya Msumbiji .

Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dr.Hussein Ngaillah anasema Hospitali hii, iliyoanza kutoa huduma rasmi mnamo Juni 2021, imeleta mapinduzi makubwa katika sekta ya afya, ikihudumia kata 20 zenye jumla ya wakazi 191,193, wakiwemo wanawake 93,494 na wanaume 97,699, pamoja na vijiji vya jirani kutoka Halmashauri ya mji wa Mbinga na  nchi jirani ya Msumbiji.

HUDUMA ZINAZOPATIKANA

Kwa kipindi cha takriban miaka mitatu tangu kuanzishwa kwake, Hospitali ya Nyasa imefanikiwa kutoa huduma mbalimbali muhimu kwa jamii. 

Huduma hizi ni pamoja na wagonjwa wa nje (OPD), wagonjwa wa ndani (IPD), huduma za maabara, afya ya uzazi na mtoto (RCH), dawa na vifaa tiba, huduma za mionzi kama X-ray na Ultrasound, afya ya kinywa na meno, fiziotherapia, na matibabu ya dharura (EMD).

Zaidi ya hayo, hospitali inatoa huduma za afya msonge, ikiwemo matibabu ya kifua kikuu na ukoma, tohara kwa wanaume, uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi, pamoja na chanjo mbalimbali kama ile ya homa ya ini na chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi.

ONGEZEKO LA WAGONJWA NA MAENDELEO YA HUDUMA

Tangu kuanzishwa kwake, hospitali hii imekuwa ikishuhudia ongezeko kubwa la wagonjwa wanaohudumiwa. Katika mwaka wa fedha 2020/2021, hospitali ilihudumia wagonjwa 195 pekee. 

Hata hivyo, idadi hii iliongezeka maradufu mwaka wa fedha 2021/2022 kufikia wagonjwa 3,325. Mwaka uliofuata wa 2022/2023 idadi iliongezeka hadi wagonjwa 6,907, na mwaka wa fedha 2023/2024 hospitali ilihudumia wagonjwa 10,374. Ongezeko hili linaonesha jinsi hospitali hii inavyoendelea kuwa tegemeo kubwa kwa jamii.

UJENZI NA MAENDELEO YA MIUNDOMBINU

Hospitali ya Wilaya ya Nyasa imekuwa ikipanuka kwa awamu tatu chini ya mfumo wa Force Account, kwa kutumia jumla ya shilingi 3,391,376,520.00 kutoka Serikali Kuu.

Awamu ya Kwanza (2018/2019): Ujenzi wa majengo saba ukiwemo jengo la utawala, jengo la wazazi, jengo la wagonjwa wa nje, huduma za mionzi, ufuaji, stoo ya dawa na maabara kwa gharama ya shilingi 1,800,000,000.00.

Awamu ya Pili (2020/2021): Ujenzi wa wodi tatu (watoto, wanawake, na wanaume) pamoja na kichomea taka kwa gharama ya shilingi 491,376,520.00.

Awamu ya Tatu (2021/2022): Ujenzi wa jengo la upasuaji, wodi za upasuaji kwa wanaume na wanawake, jengo la kuhifadhi maiti, na jengo la huduma za dharura (EMD), kwa jumla ya shilingi 1,100,000,000.00 kutoka Mfuko wa Maendeleo wa Taifa wa UVIKO-19 (IMF).

UJENZI WA KITUO CHA KUFUA HEWA TIBA (OXYGEN PLANT)

Katika mwaka wa fedha 2023/2024, hospitali hii ilipokea mradi mkubwa wa uzalishaji wa hewa tiba (Oxygen Plant), uliotekelezwa na Serikali Kuu kupitia Wizara ya Afya na OR-TAMISEMI kwa gharama ya shilingi 409,000,000.00. Ufungaji wa mfumo huu ulifanywa na kampuni ya Tanzania Oxygen Gases Ltd, ukihusisha majengo ya huduma za dharura, wodi za upasuaji, na jengo la wazazi.

UWEKEZAJI KATIKA VIFAA TIBA

Katika kuhakikisha huduma bora zinaendelea kutolewa, Serikali imewekeza shilingi 1,208,105,000.00 katika ununuzi wa vifaa tiba kupitia Bohari Kuu ya Dawa (MSD).

 Mwaka wa fedha 2021/2022: Vifaa vyenye thamani ya shilingi 490,000,000.00 vilinunuliwa 

Mwaka wa fedha 2023/2024: Vifaa vya shilingi 418,105,300.00 kwa ajili ya jengo la EMD na Mwaka wa fedha 2024/2025: Vifaa vya shilingi 300,000,000.00 vinatarajiwa kusambazwa.

Hospitali ya Wilaya ya Nyasa imepiga hatua kubwa katika kutoa huduma bora kwa wananchi, huku Serikali ikiendelea kuwekeza katika miundombinu na vifaa tiba. 

Kwa maendeleo haya yanayoendelea, ni dhahiri kuwa Hospitali ya Wilaya ya Nyasa inaelekea kuwa moja ya  hospitali za kisasa zinazotoa huduma bora kwa wananchi, ikiwa ni matokeo ya jitihada kubwa za  uwekezaji uliofanywa na Serikali .

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.