• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HOSPITALI ya Wilaya ya Namtumbo ukombozi wa wajawazito na watoto

Imewekwa kuanzia tarehe: September 2nd, 2020

SERIKALI  imekamilisha ujenzi wa majengo nane ya hospitali ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma ambapo  kazi iliyokuwa imebaki ya  kuunganisha mfumo wa umeme  na maji safi imekamilika.

Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Dr.Godwin Luta anasema Halmashauri hiyo,imekamilisha ujenzi wa hospitali ya wilaya ambao umetokana na jitihada za serikali  ya awamu ya Tano za kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma ya matibabu jirani na maeneo wanayoishi.

Serikali inayoongozwa na Rais Dkt.John Magufuli imedhamiria kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi na kuwekwa msisitizo kwenye ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015 ambapo hadi sasa vimejengwa vituo vya afya na hospitali katika maeneo mbalimbali nchini.

“Ujenzi huu umefanyika kwa awamu tano ambapo kwa mwaka 2010/2011,Halmashauri yetu ilipokea fedha kutoka serikali kuu kiasi cha shilingi milioni 450 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala na wagonjwa wa nje’’,anasema Dr. Luta.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Venance Nachimbinya  anabainisha zaidi kuwa kati ya fedha zilizotolewa,katika jengo la wodi ya wazazi zimetumika zaidi ya shilingi milioni 176 na jengo la wodi ya wanaume zimetumika zaidi ya shilingi milioni 259.

Anabainisha zaidi kuwa jengo la upasuaji limegharimu zaidi ya shilingi milioni 213,jengo la stoo ya dawa zaidi ya shilingi milioni 203,jengo la maabara milioni 164,jengo la kufulia zaidi ya milioni 113,jengo la mionzi zaidi ya milioni 136,jengo la wodi ya wanawake zaidi ya milioni 166 na jengo la watoto zaidi ya milioni10.


Christina Mndeme ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma anawaagiza watendaji wa Halmashauri ya Namtumbo  kuhakikisha majengo yaliyokamilika yanaanza kutumika kutoa huduma kwa wananchi wa Namtumbo ili kutimiza azma ya serikali ya kusogeza huduma ya afya karibu na wananchi.

“Wananchi hawataki kuona majengo. Badala yake wanataka kupata huduma za afya katika hospitali ,serikali imetekeleza wajibu wake wa kutoa fedha za kukamilkisha ujenzi ’’,anasisitiza Mkuu wa Mkoa.

 John Milazi Mkazi wa Namabengo anasema kutekelezwa kwa mradi huo kunamfanya ajisikie amani kwa sababu akinamama na watoto kwa miaka mingi walikuwa wanapata shida  ambapo hivi sasa serikali imewakumbuka kwa  kuwajengea hospitali yenye huduma zote muhimu.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Septemba Mosi,2020


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.