• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAHAWA za maganda kusafirishwa nje ya nchi zitakavyoathiri viwanda vya kukoboa kahawa Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: March 14th, 2023

BAADHI ya viwanda vya kukoboa kahawa katika wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma,viko hatarini kufungwa kutokana na kupungua kwa uzalishaji na bodi ya Kahawa Tanzania kuruhusu makampuni  na wafanya biashara binafsi kusafirisha kahawa kavu kwenda nje ya wilaya hiyo.

Wamiliki wa viwanda hivyo, wameiomba bodi ya Kahawa Tanzania kutoruhusu makampuni na wafanyabiashara hao kusafirisha kahawa ghafi(za maganda) ili kulinda viwanda  vilivyopo katika wilaya hiyo badala yake  kahawa yote ikobolewe kwenye viwanda vya Mbinga.

Wamesema,kama Serikali kupitia Bodi ya Kahawa Tanzania itaendelea kutoa vibali katika msimu  huu basi kuna uwezekano mkubwa wa viwanda vya Mbinga kufungwa kwa kukosa malighafi na  hata kusababisha watu wengi hususani vijana kukosa ajira.

Meneja Uzalishaji wa kiwanda cha kukoboa kahawa cha MCCCO Rabiel Ulomi alisema,wilaya ya Mbinga kuna viwanda vitatu vyenye uwezo wa kukoboa tani  tani elfu hamsini,lakini tangu wilaya hiyo ilipoanzishwa uzalishaji wa zao hilo haujafikia kiwango hicho.

Alisema,kiwanda cha MCCCO kina uwezo wa kukoboa tani 30,000 kwa mwaka ambapo katika msimu wa 2022/2023 kimekoboa tani 8,846 na kilo 647  chini ya malengo ya kukoboa angalau tani 10,000.

Alisema,hali hiyo imetokana na kushuka kwa uzalishaji na Bodi ya kahawa kuruhusu makampuni yanayonunua kahawa kutoka kwa wakulima kupeleka nje, badala ya kutumia viwanda vya ndani ya wilaya hiyo.

Alisema,hatua hiyo imeathiri sana viwanda vya Mbinga,uchumi wa wananchi wa Mbinga na wilaya hiyo ambao kwa kiasi kikubwa inategemea mapato na uchumi wake kutoka kwenye viwanda hivyo.

Ulomi ameishauri serikali  kuhakikisha kuwa,kahawa inayolimwa Mbinga inaborewe kwenye viwanda vilivyopo katika wilaya hiyo badala ya kupelekwa nje na mkulima akishaingiza kahawa kiwandani aendelee na mchakato hadi siku ya mnada.

Mmiliki wa kiwanda kingine ambaye hakutaka kutaja jina lake alisema,kama bodi ya kahawa itaendelea kuruhusu kahawa ya Mbinga kusafirishwa na kwenda kukobolewa nje,kuna uwezekano mkubwa wa viwanda vya Mbinga kufungwa.

Aidha,ameiomba serikali kupitia upya uamuzi wake wa kuruhusu jambo hilo,kwani lina madhara makubwa kwa wananchi na wilaya ya Mbinga ambayo inategemea zao la kahawa kama nguzo kuu ya kiuchumi.

Mmoja wa  vibarua katika kiwanda cha MCCCO Daud Challe alisema,kama Bodi ya kahawa itaruhusu kahawa ya Mbinga isafirishwe na kukobolewa nje ya viwanda vya Mbinga,basi Taifa litegemee kuongezeka kwa vijana wengi wa mitaani ambao hawana ajira.Alisema utaratibu huo ukisitishwa,uchumi wa Mbinga utaongezeka na wananchi watapata ajira kupitia  shughuli mbalimbali zinazofanyika kwenye viwanda vya kukoboa kahawa.

Kwa upande wake meneja wa Bodi ya Kahawa kanda ya Songea Peter Bubelwa alisema,kampuni inayolalamikiwa kununua na kusafirisha kahawa nje ya Mbinga,imepata  vibali kutoka Halmashauri  zote zinazolima zao hilo ambazo zimeridhia utaratibu huo.

“ni kweli kuna viwanda vitatu katika wilaya ya Mbinga vyenye uwezo mkubwa wa kukoboa kahawa yote inayozalishwa,lakini sisi kama bodi ya kahawa tumeruhusu kampuni  hiyo(Aviv Ltd) ambayo ni mdau na mkulima mkubwa kununua na kusafirisha kahawa nje ili kuleta ushindani  katika sekta ya kahawa”alisema Bubelwa.

Naye mtaalam kutoka Bodi ya kahawa Tanzania kanda ya Songea Rashid Membe alisema,kilio cha wamiliki wa viwanda vya kukoboa kahawa ni kuendelea kuwahimiza wakulima kuongeza uzalishaji wa zao hilo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.