• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAMBI ya uchunguzi wa magonjwa ya macho kufanyika Ruvuma kwa siku kumi

Imewekwa kuanzia tarehe: November 12th, 2024

Daktari Bingwa wa Macho kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Songea (HOMSO) Dr. Charles Hinju, amesema wameungana na madaktari bingwa kutoka ndani na nje ya nchi kutoa matibabu ya macho kwa wakazi wa Ruvuma.

Amesema huduma hizo zinazotolewa kwa gharama nafuu kupitia shirika la EyeCorps, kwa kushirikiana na madaktari kutoka CCBRT, Hospitali ya Kanda ya Mbeya, na Muhimbili zimeanza Novemba 11 na zitamalizika Novemba 20 katika hospitali ya Mkoa.

"Tunatoa huduma kwa gharama nafuu zaidi, watu walikuwa wanakuja kwetu na wanakosa huduma kwa kukosa kuchangia gharama, lakini hawa ndugu zetu na kwa kushirikiana na Serikali imeweza kutumia hii nafasi kupunguza gharama ndio maana watu wengi wamejitokeza kupata huduma," alisema Dr. Hinju.

Ameongeza kuwa katika kipindi cha wiki moja kabla ya kuanza rasmi matibabu hayo madaktari walitembelea Vijiji vya Wilaya ya Namtumbo, Songea Vijijini, na Manispaa ya Songea, kuwachunguza wagonjwa na kufanikiwa  kuwapata wagonjwa zaidi ya 1,000.

Amebainisha kuwa wanatarajia kufanya upasuaji wa mtoto wa jicho kwa watu 250, na huduma zingine kama kutoa miwani kwa wenye shida ya kuona, kusoma maandishi, na mwanga zinatolewa, hivyo wananchi waendelee kujitokeza ili waweze kufaidika na huduma hiyo.

Mmoja kati ya wagonjwa waliopatiwa huduma ya macho Florencia John kutoka Wilaya ya Tunduru amesema amefurahishwa na huduma aliyopatiwa kwa sababu alikuwa na tatizo kwenye macho yote mawili na ameshahudumiwa jicho moja na ameanza kuona, amewaomba watoa huduma kuendelea kutoa huduma hizo kwa kuwa sio kila mtu anaweza kulipia.

Naye Selemani Sindo kutoka Wilaya ya Namtumbo ameeleza kuwa jicho lake moja lililkuwa halina uwezo wa kuona lakini baada ya upasuaji sasa anaona vizuri kwa kutumia macho yote.

Huduma hii inayotolewa na kambi ya madaktari wa uchunguzi wa magonjwa ya macho huwa inatolewa kila mwaka  ambapo mwaka 2023 wagonjwa 185 mkoani Ruvuma walipatiwa matibabu ya upasuaji wa mtoto wa jicho, na mwaka huu wanatarajia kufanya upasuaji huo kwa watu 250.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.