• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KATIBU Tawala Ruvuma ashauri ushirikiano kutokomeza ukatili

Imewekwa kuanzia tarehe: December 4th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Mary Makondo, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya wazazi, serikali, na wadau mbalimbali katika kupinga ukatili wa kijinsia na kuhakikisha haki za watoto na wanawake zinalindwa.

Amesisitiza hayo wakati akizindua siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ambapo uzinduzi huo kimkoa umefanyika katika wilaya ya Namtumbo.

"Kama mkoa kwa pamoja tunatakiwa kuhakikisha tunapinga ukatili kwa nguvu zote, kila mzazi kutimiza wajibu wake kwenye malezi na kuhakikisha watoto wanapata haki zao bila kujali jinsia zao, mgawanyo wa kazi, fursa za kupata Elimu, kutoa ushauri na kusikilizwa viwe sawa," alisema Bi. Mary.

Ameongeza kuwa wanawake wanapaswa kushiriki katika maamuzi na shughuli za kiuchumi bila kuathiri majukumu yao kama walezi wa familia, kwani watoto wamekuwa wakijilea wenyewe kwenye maeneo mengi ya mkoa wa Ruvuma, hali inayochangia kuongezeka kwa vitendo vya ukatili kutokana na ukosefu wa ulinzi na usalama wa kutosha.

Bi. Mary amesema Serikali imekuwa ikifanya kazi nzuri lakini inakosa ushirikiano katika kutoa Elimu inayohusu ukatili wa kijinsia kwa sababu changamoto ya ukatili imekuwa ikiendelea.

"Upande wa Serikali tunafanya kazi nzuri sana lakini tunakosa ushirikiano kwenye kutoa Elimu na kushughulikia masuala ya ukatili kwani Elimu imekuwa ikitolewa lakini bado changamoto ya ukatili imekuwa ikiendelea, ni vyema sekta zote kuhakikisha zinafanya kazi kwa pamoja na mifumo isomane katika kushughulikia masuala ya ukatili," alisema Bi. Mary.

Kuelekea maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Bi. Mary amewahimizwa wadau kushiriki kwenye makongamano, mikutano, na mijadala kuanzia ngazi ya familia ili kujua hatua zilizopigwa na wapi palipokosewa ili kurekebisha na kuendelea kulinda haki za kila mmoja kwenye jamii.

Kauli mbiu ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia mwaka huu inasema "Kuelekea Miaka 30 ya Beijing: Chagua Kutokomeza Ukatili wa Kijinsia," ambapo mwaka 1995 wanawake wapatao 51,000 kutoka nchi mbalimbali duniani walikutana nchini China kujadili na kuweka mikakati ya kumaliza ukatili wa kijinsia.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.