• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KILA Wilaya mkoani Ruvuma ina vivutio vya utalii

Imewekwa kuanzia tarehe: September 14th, 2024

Utafiti umebaini karibu kila wilaya iliyopo katika Mkoa wa Ruvuma ina vivutio mbalimbali vya utalii vinavyoweza kufungua milango ya utalii katika wilaya husika na kutoa ajira kwa vijana kupitia sekta hiyo adimu hapa nchini na duniani kote.

Hebu tuone baadhi ya vivutio vya utalii ambavyo vipo kila wilaya mkoani Ruvuma, tukianza na wilaya ya Nyasa mjini Mbambabay kuna  fukwe, visiwa, samaki wa mapambo, hifadhi ya Ndengere, utalii wa michezo ya majini na majengo ya malikale ya makanisa ya Lituhi na Lundu.

Eneo la Liuli wilayani Nyasa kuna vivutio vya Jiwe la kihistoria la Pomonda, fukwe, samaki wa mapambo, historia ya kanisa la Anglikana   Tanzania, michezo ya majini, ngoma za asili  za kioda na mganda.

Katika eneo la Lundu wilayani humo, kuna vivutio vya jiwe la Chingata, fukwe za samaki wa mapambo, hifadhi ya misitu ya asili ya Lilengalinga, majengo ya historia, michezo ya majini na ngoma za asili.

Wilaya ya Mbinga,nayo imebarikiwa kuwa na vivutio vingi vya utalii vikiwemo bustani ya wanyama ya Lugari, jiwe la maajabu la Mbuji,kilimo cha Ngoro na pori la Liparamba ambalo linafaa kwa utalii wa picha,utafiti wa mimea na utalii wa uwindaji.Maeneo mengine ya utalii katika wilaya ya Mbinga ni Hifadhi.

Tukiangalia katika wilaya ya Songea,kuna Hifadhi ya Gesimasowa ambayo  inafaa kwa utafiti wa aina mbalimbali, kuwinda na utafiti wa malikale,Hifadhi ya asili ya Luhira, Hifadhi ya Misitu ya milima ya Matogoro,Makumbusho ya Taifa ya Majimaji, Makumbusho ya Mzee Kawawa na Pango la Mlima Chandamali ambalo lilikuwa maficho ya Nduna Songea Mbano wakati wa Vita ya Majimaji.

Vivutio vingine vilivyopo katika wilaya ya Songea ni Bwawa la Tulila, maporomoko ya Mto Ruvuma, majengo na majumba ya kihistoria likiwemo kanisa kongwe la Peramiho.

Vivutio vya utalii vilivyopo katika wilaya ya Tunduru ni  Hifadhi ya Taifa ya Nyerere kanda ya Kalulu linalofaa kwa utalii wa uwindaji, Hifadhi ya asili ya Mwambesi inayofaa kwa utalii wa picha na utafiti, eneo la utalii wa mambokale la Masonya na njia ya kusafirishia watumwa ya Mbatamila hadi Masonya ambako ilikuwa kambi ya wakimbizi na ofisi za vyama vya FRELIMO toka Msumbiji.

Katika wilaya ya Tunduru pia kuna njia ya watumwa ya Kusini iliyokuwa inapitisha watumwa toka Msumbiji kupitia mkoa wa Ruvuma hadi Mikindani mkoani Mtwara ambako kulikuwa na soko la watumwa.

Katika wilaya ya Namtumbo kuna vivutio vya utalii ambavyo ni  Hifadhi ya Taifa ya Nyerere Kanda ya Likuyuseka ambayo inafaa kwa uwindaji wa utalii na utalii wa picha na Mji mdogo wa  Lusewa katika maeneo ya Kimbanda na Kisungule ambako kunafaa kwa utalii wa kuwinda na picha.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.