Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ally Senga Gugu, amefungua rasmi Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma chenye hadhi ya Daraja B, kilichojengwa kwa gharama ya Shilingi milioni 798
. Ujenzi wa kituo hicho ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuboresha miundombinu ya usalama nchini.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Katibu Mkuu Gugu alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake mahiri unaotoa kipaumbele kwa sekta ya usalama.
Aidha, alimshukuru Mbunge wa Jimbo la Namtumbo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Vita Kawawa, kwa mchango wake mkubwa katika kufanikisha mradi huo.
Gugu alieleza kuwa katika kipindi cha miaka minne iliyopita, Serikali imeongeza juhudi kubwa katika kuboresha mazingira ya kazi kwa askari polisi, kwa kujenga na kukarabati vituo vya polisi nchini, hatua inayolenga kuimarisha huduma za ulinzi kwa wananchi. Alisisitiza kuwa ujenzi wa kituo hicho ni mfano wa namna Serikali inavyowekeza katika usalama wa wananchi wake.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.