• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAAGIZO mazito ya RC Ibuge kwa TANROADS Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: February 22nd, 2022

MKUU wa mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge,amekagua Daraja la Mto Muhesi wilayani Tunduru na kuiagiza wakala wa Barabara Tanroads mkoa huo, kusimamia matumizi sahihi ya mizani na kuwachukulia hatua kali madereva wanaozidisha uzito kwenye magari na baadhi ya watu wanaoiba na kuharibu kwa makusudi alama za barabara.

Brigedia Jenerali Ibuge,ametoa agizo hilo alipotembelea daraja la Mto Muhesi wilaya ya Tunduru ambalo baadhi ya miundombinu yake imeharibika baada ya kufunikwa na maji kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha wilayani humo na mikoa jirani.

Mkuu huyo wa mkoa,amemuagiza meneja wa Tanroads mkoa wa Ruvuma Mhandisi Ephatar Mlavi kufanya tathimini ya athari iliyotokea na kufanya matengenezo ya haraka kwa kuwa daraja hilo ni muhimu kwa uchumi wa Ruvuma na mikoa mingine ya Lindi na Mtwara ili wananchi waendelee na shughuli zao za maendeleo.


Amewataka,madereva wanaoendesha magari ya abiria na malori kuzingatia sheria kwa kuepuka kuzidisha uzito ili kulinda barabara na miundombinu yake inayojengwa kwa gharama kubwa na Serikali.

Alisema, barabara ya Songea-Namtumbo hadi Tunduru ina muda mfupi takribani miaka mitano tangu ilipojengwa,lakini baadhi ya maeneo imeanza kuharibika na hali hiyo inatokana na madereva wasiozingatia sheria kwa kuzidisha uzito katika magari yao.

Aidha ameiomba Wizara ya ujenzi na Uchukuzi kupitia wakala wa Barabara Tanroads makao makuu, kujenga mizani nyingine kati ya Songea na Tunduru ili kudhibiti uzito wa magari.

Alisema, sehemu kubwa ya barabara hiyo hakuna udhibiti wa uzito wa magari badala yake kutegemea mizani ya Makambako na Tunduru tu ambazo zinatoa nafasi kwa madereva wasio waaminifu kuongeza mizigo njiani tofauti na ile iliyokaguliwa kwenye mizani hizo.


Ibuge,amewataka wananchi wa mkoa wa Ruvuma na watumiaji wengine wa barabara hiyo kuzingatia sheria na kuepuka kufanya shughuli za kibinadamu kando kando ya barabara kwani tabia hiyo inachangia sana kuharibu miundombinu ya barabara.
Brigedia Jenerali Ibuge,amempongeza Mkuu wa wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro na meneja wa Tanroad mkoa kwa hatua walizochukua kuzuia magari na watu kupita kwenye daraja hilo kwani uamuzi huo umesaidia kuzuia kutokea kwa madhara makubwa.
Kwa upande wake Meneja wa Tanroads mkoa wa Ruvuma Mhandisi Ephatar Mlavi alisema, baada ya kufanya ukaguzi wamebaini kipande kimoja cha daraja kimetoka sehemu yake,lakini wameruhusu kutumika kwa upande mmoja ili kutoa nafasi kwa wananchi kuendelea na shughuli zao.

Mlavi alisema, wameshatoa taarifa makao makuu ambapo vifaa na wataalam wameanza safari ya kuja eneo hilo kwa ajili ya kufanya marekebisho kipande kilichohama.
Mkuu wa wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro alisema, mvua zilizonyesha katika mikoa ya jirani zilileta maji mengi katika Mto Muhesi na kusababisha daraja hilo kufunikwa na maji hali iliyosababisha usafiri kati ya mikoa ya Lindi,Mtwara kuelekea Ruvuma kusimama kwa muda.

Kwa mujibu wa Mtatiro,baada ya maji kupungua kamati ya ulinzi na usalama na ofisi ya Tanroads kufanya ukaguzi wa kina wameruhusu daraja hilo kutumika huku wakisubiri wataalam kwenda kufanya marekebisho ya kipande kilichoathirika.
Alisema,barabara ya Songea-Namtumbo-Tunduru hadi Mangaka mkoa jirani wa Mtwara mizani inayotumika kudhibiti uzito wa magari iko Tunduru tu jambo linalotoa nafasi kwa madereva wasiotaka kutii sheria kuongeza mizigo njiani,jambo lililochangia sehemu ya barabara hiyo kuanza kuharibika haraka.
MWISHO.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.