• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAAGIZO ya Makamu wa Rais kwenye maonesho ya nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini

Imewekwa kuanzia tarehe: August 3rd, 2023

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amekemea tabia ya uvamizi na mtindo wa kubadili matumizi ya ardhi iliyotengwa mahususi kwa ajili ya Utafiti wa Kilimo.

Makamu wa Rais ametoa maagizo hayo wakati akifungua maonesho ya Nane nane kitaifa yanayofanyika katika viwanja vya John Mwakangale mkoani Mbeya. Amesema maeneo mengi ya taasisi za utafiti yamevamiwa na kupimwa viwanja jambo ambalo linatishia utafiti wa kilimo na mifugo kwa kuwa vituo vya utafiti vitakosa maeneo ya kutosha ya kufanyia kazi.  

Makamu wa Rais amewataka watanzania kutambua kilimo ni sayansi na hivyo utafiti kilimo usipopewa kipaumbele basi mapinduzi ya kilimo yatabaki kuwa ndoto. Amesisitiza umuhimu wa kupima maeneo ya taasisi za utafiti wa kilimo, kupewa hati na kulindwa wakati wote. Vivyo hivyo ameelekeza mamlaka zinazohusika kutenga na kupima ardhi katika maeneo ya uzalishaji wa mbegu na kuyalinda dhidi ya uvamizi.

Vilevile Makamu wa Rais amekemea uwepo wa makundi makubwa ya mifugo yalioingizwa katika mikoa ya nyanda za juu kusini. Amesema madhara yake ni makubwa ikiwemo kuharibiwa sana kwa mazingira kuongezeka kwa migororo mingi kati ya wakulima na wafugaji, wanyama kama Tembo kukimbia bugudha ya mifugo na kuhamia kwenye makazi ya binadamu wakiharibu mazao na hata kuua watu. Amezitaka Wizara zote husika na Wakuu wa Mikoa kuchukua hatua thabiti kudhibiti uingizaji mifugo kinyemela katika maeneo yao ya utawala.

Makamu wa Rais ametoa wito kwa wakulima, wafugaji na wavuvi kuzingatia maelekezo ya wataalam ili kuweza kuzalisha pasipo kuathiri afya ya binadamu na mazingira kutokana na kuongezeka kwa matumizi yasiyo sahihi ya viuatilifu na kemikali nyingine jambo lenye athari kubwa kwa afya ya binadamu na viumbe hai vingine.

Ameongeza kwamba Serikali inaendelea kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji nchini ikiwemo kujenga mabwawa ya kuvuna maji ya mvua kwa ajili ya umwagiliaji, ambapo lengo ni kufikia eneo la umwagiliaji la hekta 1,200,000 ifikapo mwaka 2025. Pia ametoa wito kwa wananchi kutumia na kutunza miundombinu hiyo ili iweze kutumika kwa muda mrefu na kusaidia kuleta tija.

Makamu wa Rais ametoa rai kwa wakulima kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula ili taifa liweze kujitosheleza kwa chakula na kupata fedha zaidi za kigeni kutokana na mazao mbalimbali. Amasema Serikali kwa upande wake itaendelea kuimarisha utoaji wa huduma za ugani kwa kuwapatia Maafisa Ugani vitendea kazi mbalimbali vikiwemo pikipiki, vifaa vya matibabu, uhimilishaji pamoja na vifaa vya kupima afya ya udongo.

Ameitaka Wizara ya Kilimo na Mifugo kuanza maandalizi ya kuchukua vijana wengine katika programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (Building a Better Tomorrow - BBT) pamoja na kuziagiza Wizara za Kilimo na Mifugo na Uvuvi kuona namna bora ya kushirikiana na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ili vijana wa JKT wanaojitolea wapewe kipaumbele kushiriki katika programu hiyo.

Makamu wa Rais ameendelea kusisitiza taasisi za fedha na mabenki hapa nchini kuendelea kushusha riba zaidi ili kuwasaidia wakulima na wafugaji. Ameitaka Wizara ya Kilimo na Fedha kufikiria kuanzishwa kwa  mfuko wa maendeleo ya kilimo utakaosaidia kushusha riba kwa wakulima, wafugaji na wavuvi.

Amewapongeza watafiti waliosaidia katika upatikanaji wa mbegu na kutoa wito kwa Wizara ya Kilimo kutafuta utaratibu wa kuwapa tuzo vijana na wabunifu wanaotoa suluhu ya mambo mbalimbali katika kilimo, ufugaji na uvuvi.

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema sekta ya kilimo inaendelea kuimarika kutokana na juhudi za serikali katika kuinua sekta hiyo ikiwemo kuongezeka kwa bajeti kufikia shilingi bilioni 970 kutoka bilioni 294. Ameongeza kwamba kuimarika kwa sekta hiyo kumepelekea kuzalishwa kwa kahawa tani 80000, tumbaku kilo milioni 120 huku uzalishaji wa pamba ukiongezeka mara mbili. Bashe ameishukuru serikali kwa kutoa shilingi bilioni 100 ili kusaidia makampuni ya pamba yaweze kununua zao hilo kwa wakulima.  

Waziri Bashe amesema maendeleo ya kilimo yanategemea ufanisi katika sekta zingine ikiwemo bandari. Ameongeza kwamba mabadiliko na uwekezaji wa tija katika bandari yanahitajika kwa sasa kwani yatasaidia wakulima katika kusafirisha mazao yao.

Pia amesema kuanzia mwaka 2024 nchi zote za Afrika zitapata mialiko ya kuhudhuria maonesho ya Nane nane huku akisisitiza mialiko hiyo haitahusisha viongozi pekee bali hadi wakulima na wanunuzi wa mazao wa nchi hizo. Ameongeza kwamba kufuatia kupanda hadhi kwa maonesho hayo kuwa ya kimataifa, juhudi mbalimbali zinaendelea ikiwemo kuboresha maeneo yanayotumika kwa ajili ya sherehe hizo kwa kuyajenga ili yawe ya kudumu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.