• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MADABA waagizwa kujenga viwanda vya kuongeza thamani mazao

Imewekwa kuanzia tarehe: November 27th, 2022

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Madaba kutenga maeneo ya kujenga viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya miti.

Kanali Thomas ametoa ushauri huo wakati anazungumza watendaji wa Halmashauri hiyo kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Madaba.

Amesema hali ya hewa ya Madaba inafaa kwa mazao ya miti,parachichi na tangawizi hivyo vikianzishwa viwanda kuongeza thamani ya mazao hayo wananchi watapata faida maradufu. “Anzisheni pia mashamba ya pamoja (block farming) ,wakulima watapata fursa ya kulima zao la aina moja hivyo kuongeza uzalishaji na kuinua uchumi “, alisema.

Mkuu wa Mkoa pia amewaagiza watendaji kuhakikisha mbolea ya ruzuku inawafikia wakulima jirani na maeneo wanayoishi.

katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amewaagiza watendaji katika Halmashauri ya Madaba kusimamia utekelezaji wa miradi ili iweze kukamilika ndani ya mkataba.

Amesema Rais Samia Suluhu Hassan anatoa mabilioni ya fedha kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo hivyo ni lazima miradi itekelezwa kwa viwango ndani ya mkataba .

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Madaba Sajidu Idrisa Mohamed amepongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya shilingi bilioni 2.1 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Halmashauri hiyo. 

Amesema hospitali ya Madaba inatarajia kuanza kutoa huduma za afya wakati wowote ambapo serikali tayari imefunga mashine ya X-ray yenye thamani ya shilingi milioni 350. 

Ameongeza kuwa katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 serikali imetoa shilingi bilioni 186 kwa ajili ya kulipa malimbikizo ya watumishi 127 katika Halmashauri ya Madaba.

Halmashauri ya Madaba yenye watumishi 616 ina upungufu wa watumishi 407. 

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma 




Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.